Tuesday, October 15, 2013

BIDHAA ZAPANDA WAKATI WA SIKUKUU SINGIDA

Na.Anna Chiganga


Kupanda kwa bidhaa hasa za vyakula hasa kwa wakati huu wa kuelekea sikuu ya Eid el haji kunatokana na ugumu wa kupatikana kwa bidhaa hizo mkoani singida
Baadhi ya wafanyabiashara wa soko kuu mkoani singida wamesema hayo wakati wakizungumza na standard redio
Mmoja wa wafanyabiashara hao aliyefahamika kwa jina la Khamisi Wadu  amesema kuwa wakazi wa singida na wanunuzi kwa ujumla hawanabudi kufahamu kuwa bidhaa zinapanda bei kutokana na kutopatikana kwa bidhaa hizo mkoani Singida
Ametaja baadhi ya vyakula ambavyo havizalishwi mkoani Singida kuwa ni pamoja na viazi mviringo (mbatata)
Ameshauri wakazi wa mkoa wa singida kuepuka dhana potofu kuwa  bidhaa zinapanda bei wakati wa sikuu bali kunatokana na ugumu wa kupatikana kwa bidhaa hizo

No comments: