Friday, October 18, 2013

WANANCHI WATAKIWA KUWAPA FURSA VIJANA YA MAWAZO KATIKA KAZI




Na.Edilitruda chami
Wananchi mkoani Singida wametakiwa kuwaheshimu vijana wanaofanya kazi katika sekta mbalimbali bila kujali umri wao ili wanufaike na matunda ya kazi hizo
Afisa ustawi wa jamii mkoa wa Singida Bw Amosi Makala baada ya kugundua  kuwa baadhi ya wananchi hawafiki  katika ofisi za ustawi wa jamii kupata ushauri nasaha pindi wanapokuwa na tatizo

Bw  Makala amesema baadhi ya watu kama vile wazee  hudharau ushauri wanaopewa na wafanyakazi vijana katika ofisi za ustawi wa jamii kwa kuangalia umri na umbo jambo ambalo ni hatari katika utendaji kazi na linalokwamisha maendeleo mkoani Singida

Amesema, ni vyema wananchi kufahamu kuwa endapo hawatafuata ushauri wanaopewa na ustawi wa jamii au kuogopa kufika ofisi hizo wanapokumbana na matatizo mbalimbali kutachangia ongezeko la vitendo vya ukiukaji wa haki za kibiinaadamu

No comments: