Thursday, October 24, 2013

DR.KONE KUKANUSHA ONGEZEKO LA WATOTO WAISHIO MAZINGIRA MAGUMU SINGIDA




Na.edson raymond

Mkuu wa mkoa wa Singida Dr. Parseko Kone amekanusha taarifa kutoka kwa baadhi ya watu wanaodai kuwa mkoa wa Singida unakabiliwa na idadi kubwa ya watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi.

kutoa ufafanuzi huo kutokana na baadhi ya washiriki waliohudhuria katika kikao cha siku maalumu ya polisi kudai kwamba mkoa wa singida unakabiliwa na idadi kubwa ya watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi

Aidha amesema tangu mwaka 2008 mkoa wa singida umekuwa ukipambana na changamoto hiyo ya watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi

Amesema mafanikio ni makubwa kwani mkoa kwa kushirikiana na shirika la kimataifa la Outreach International umefanikiwa kujenga kituo cha Kids Center kinachotumika kuwapatia huduma muhimu watoto hao.

Dr Kone ametoa wito kwa wakazi wa mkoa wa singida kuwakamata watoto hao pindi wanapowaona na kuwafikisha katika kituo hicho, kwani kimejengwa kwa ajili ya kutoa huduma muhimu kama vile elimu ya awali, na mahitaji mengine

No comments: