Friday, October 18, 2013

WAZAZI TUPIGE VITA UMASKINI MARADHI NA UJINGA KWA WATOTO WETU





 Na.Emanuel gamasa
 Wazazi wametakiwa kufuata misingi ya baba wa taifa mwalimu Julius Nyerere kwa kupiga vita umaskini,maradhi na ujinga kwa kuwahimiza watoto kuhudhuria  shule na kufuatilia maendeleo yao ya kitaaluma pindi wawapo shuleni

Kaimu mkuu wa magereza wa mkoa wa Singida Titus Mbuta amesema hayo katika mahafali ya darasa la saba katika shule ya msingi Ititi iliyopo manispaa ya singida
Amesema iwapo wazazi watafuata misingi ya baba wa taifa kwa kupiga vita umaskini, maradhi na ujinga kwa kuhakikisha  watoto wao wanapata elimu ya kutosha na itakayo wanufaisha katika maisha yao
Kwa upande mwingine amewataka wazazi kuwa na ushikiano na walimu ili kuhakikisha watoto wao wanasoma kwa bidii na kutokomeza utoro


No comments: