Thursday, October 24, 2013

WAJAWAZITO WATAKIWA KUHUDHURIA KLINIKI




 Na.abdul bandola
Akina mama wajawazito wametakiwa kuwahi hosipitalini  ili kuepuka  mazingira yanayoweza kusababisha matatizo makubwa wakati wa kujifungua

Mratibu wa mradi wa JIDA unoshugulikia masuala ya wanawake na watoto Bi Amina Macona kutoka wilaya ya Igunga mkoani Tabora  amesema hayo katika semina iliyozishirikisha asasi zisizo za kiserikali katika ukumbi wa Kanisa la  kkkt la Msalaba mrefu mkoani Singida.
Amesema  kuwa iwapo watakuwa karibu na vituo vya kutolea huduma wataepuka vifo visivyo vya lazima kwa akina mama

Aidhsa amesema upatikanaji wa huduma kwa akina mama nihafifu kutokana na uelewa mdogo miongoni mwa akina mama nchini.
Kwa upande mwingine Bi Amina amesema kutokana na baadhi ya akina mama kuwa hatakama wanakadi za CHF na Imani potofu  husababisha baadhi ya wanawake kutofika katika vituo vya afya

No comments: