Tuesday, October 15, 2013

WATU ELFU MBILI WAKAMATWA NA DAWA ZA KULEVYA

Na Imani Musigwa.
Watu elfu mbili wamekamatwa katika kipindi cha kuanzia  Januari hadi September mwaka huu wakituhumiwa kujihusisha na usafirishaji na utumiaji wa dawa za kulevya
Takwimu hizo zimetolewa na  Rais Jakaya Kikwte wakati akihutubia katika kilele cha mbio za mwenge wa uhuru, wiki ya vijana na maadhimisho ya miaka 14  tangu afariki baba wa taifa hayati mwalimu Julius Nyerere
Amesema licha ya kukamatwa kwa watu hao pia dawa za aina mbalimbali zimekamatwa ikiwa ni pamoja na kilo 681 zaheloin
Aidha amezipongeza nchi ambazo zimekuwa msitari wa mbele katika mapambano dhidi ya dawa za kulevya  na kuomba ushirikiano huo kuendelea kwa kuwa vita dhidi ya dawa za kulevya vinahitaji mshikamano

No comments: