Tuesday, October 29, 2013

MAHAFALI YA KUFUNGWA KWA MAFUNZO YA MGAMBO SINGIDA



Na.Edson Raymond
Kaimu mshauri wa mgambo wilaya ya Singida Ramadhan Njera ametoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Singida kujitokeza katika viwanja vya peoples kwa ajili ya kuishuhudia mahafali ya kufungwa kwa mafunzo ya mgambo tarafa ya unyakumi.

Njera ameyasema hayo leo wakati akizungumza na standard radio  ofisini kwake, ambapo amesema kuwa shughuli hiyo itaanza kesho kuanzia saa mbili na nusu ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa mkuu wa wilaya ya Singida Mwl. Queen Mlozi.

Amesema kuwa jumla ya wahitimu 90 wakiwemo wanawake 20 wanatarajiwa kupewa nishani zao na kula kiapo mbele ya mgeni rasimi Mwl. Mlozi

Aidha amesema kuwa wananchi wanatakiwa kujitokeza ili kushuhudia shughuli nzima itakayo pambwa na burudani ya ngoma, gwaride la mwendo wa pole na haraka, maonyesho ya Singe na maonyesho ya kikundi cha kwata. 

No comments: