Tuesday, October 29, 2013

OPARESHIN KIMBUNGA KUWEKA VIZUIZI BARABARANI.

Na.Imani Musigwa
Serikali imeiagiza mikoa jirani na ile inayofanya oparationi kimbunga kuweka  vizuizi vya barabarani ili kuimalisha doria na kufanya misako katika  nyumba za kulala wageni ili kuwabaini na kuwarudisha makwao wahamiaji haramu

Naibu waziri wa mambo ya ndani Bw Pereila  Silima amesema serikali imeweka mikakati mbalimbali ili kukabiliana na tatizo la wahamiaji haramu wasiotaka kurejea makwao ama wanaorejea kwa siri
Wakati huo huo serikali imesema itachunguza na kuchukua hatua stahiki  kwa watendaji waliohusika katika kuwaondoa wahamiaji kinyume na  haki za binadamu katika zoezi la operation kimbunga linaloendelea
Waziri wa ulinzi na jeshi la kujenga taifa shamsi Vuai Nahodha  amesema hayo wakati akijibu  swali la mkuu wa kambi ya upinzani bungeni mjini Dodoma Bw Freeman Mbowe  aliyetaka kujua serikali itachukua hatua gani endapo itagundulika kuwepo kwa uvunjifu wa haki za biandamu katika zoezi hilo

No comments: