Tuesday, October 15, 2013

WATANZANIA WATAKIWA KUDUMISHA UMOJA NA MSHIKAMANO



Waziri wa usitawi wa jamii maendeleo ya vijana wanawake na watoto  
wa zanziber Zainabu  Omari Mohamed  amesema zipo jitihada za kutaka kuwagawa watanzania zinazofanywa na watu wasipenda umoja na mshikamano

Akitoa salaamu  wakati wa maadhimisho ya miaka 14 ya kifo cha baba wa taifa,kilele cha mbio za mwenge wa uhuru na wiki ya vijana Bi Mohamed amesema hali hiyo ni hatari kwa msitakabili wa taifa na umoja wa watanzania

Amesema  endapo umoja wa watanzania unaonekana hivi sasa utatoweka, tanzania kusambaratika na kila mmoja atafedheheka na kuchekwa na dunia nzima

Amesema hayati baba wa taifa Mwl Julius Nyerere na Abed Aman Karume waliacha umoja ambao umekuwa mfano wa kuigwa duniani hivyo ili kuwaenzi hatunabudi  kuulinda,na  kuuendeleza mshikamano wa watanzania uliopo

Aidha amewataka watanzania  kutotoa nafasi kwa watu wanaopenda vyeo na madaraka yanayoashirika kuvuruga amani iliyojengeka kwa miaka mingi

No comments: