Thursday, October 17, 2013

JUMLA YA TANI MILIONI 13.34 ZA CHAKULA ZIMEZALISHWA KWA MWAKA 2012/2013

Na.Beatrice Moses
Waziri wa nchi Nchi Ofisi ya Rais Mahusiano na Uratibu, Steven Wasira  amesema jumla ya tani milioni 13.34 za chakula zimezalishwa kwa mwaka 2012/2013

Wasira amesema hayo jana wilayani Hanang Mkoani Manyara kwenye maadhimisho ya siku ya chakula duniani na kufafanua kuwa kiasi hicho kimetosheleza kwa asilimia 112

Amesema Serikali imejipanga kununua tani laki mbili za mazao ya nafaka baada ya kubaini kuwa wilaya 61 nchini zinakabiliwa na upungufu wa chakula

Naye kaimu mkuu wa mkoa wa manyara Bw. Khalid Mandia amesema mwaka huu mkoa huo umevuna zaidi ya tani laki tano za chakula

No comments: