Wednesday, October 23, 2013

WAHUKUMIWA MIAKA 30 KWA KUTEKA MAITI





majambazi wakipelekwa magereza baada ya kuteka maiti



Na.Edilitruda chami
Watu wanne wamehukumiwa kifungo cha miaka 30 Jela kwa kosa la unyanganyi wa zaidi ya shilling milioni nane kwa kutumia silaha

Akisoma hukumu hiyo hakimu mfawidhi wa mahakama ya wilaya mkoani Singida Flora Ndale amesema tukio hilo limetokea desember 8 waka 2012 katika barabara ya singida kwenda Dodoma maeno ya kisaki

Amesema siku ya tukio washtakiwa waliweka mawe barabarani na kuteka gari lililokua likisafirisha maiti ya mwanafuzi wa chuo kikuu cha Sokoine {SUA] kutoka morogoro kuelekea Tarime

Katika tukio hilo vitu mbalimbali kama laptop, simu za mkononi, moderm mbili zote vikiwa na thamani ya shilingi milioni nane laki saba viliibwa

Amewataja waliohukumiwa kuwa ni Hamisi Issa, Halidi Hamisi, Abbubakari Jumanne, Hamisi Alli wote wakazi wa mkoa wa Singida,ambapo siku ya tukio walikuwa na rungu,mawe na mashoka wakitumia kufanya uhalifu huo
Hakimu Ndale amesema kitendo hicho ni amesema adhabu hiyo itakua fundisho kwa watu wengine wanaofanya vitendo kama hivyo.

No comments: