Thursday, October 24, 2013

WAKAZI WA MKOA WA SINGIDA KUDUMISHA USAFI




Na.Anna chiganga
Kamati za mazingira kwenye serikali za mitaa mkoani singida zimetakiwa kuhamasisha wakazi wa mkoa wa singida kudumisha usafi katika maeneo yao kwa lengo la kuboresha manisapaa ya Singida

Akizungumza katika uzinduzi wa kamati za afya na mazingira mkurugenzi wa manspaa ya singida Bw Joseph Mchina amewataka watendaji wa mitaa na kata kuhakikisha manisipaa inakuwa katika mazingira safi na salama.

Amesema kila mtendaji wa kata atapewa lori la kubeba uchafu ili na atakayebainika kutupa taka ovyo awajibike ikiwa ni pamoja na kulipa faini

Aidha amewataka wananchi kuhakikisha wanatupa taka taka katika eneo husika pindi wanapomaliza kutumia mifuko ya Rambo ikiwa ni pamoja na kuichoma

No comments: