Thursday, October 17, 2013

HALMASHAURI ZATAKIWA KUCHUKUWA TAHADHARI YA MAGONJWA YA MILIPUKO

Na.Mwandishi wetu
Mamlaka  ya hali ya hewa Tanzania (TMA), imezitaka Halmashauri nchini pamoja na wizara ya afya,  kuchukua tahadhari ya milipuko ya magonjwa nyakati za mvua

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMA , Ibrahim Nassib, amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufunguliwa kwa warsha ya wadau mbalimbali wa mambo ya hali ya hewa na mazingira.

Amesema upo umuhimu kwa mamlaka hizo kujenga uhusiano na TMA pamoja na  kufuatilia mara kwa mara taarifa zinazotolewa na mamlaka hiyo ili kuchukua tahadhari hususani za milipuko ya magonjwa inayosabishwa  na ubovu wa miundombinu ya kupitisha maji msimu wa mvua.

Amesema milipuko mingi ya magonjwa wakati wa mvua imekuwa ikisababishwa na uchafu wa mitaro ambayo hushindwa kupitisha maji na hivyo kuzalisha wadudu wanaosababisha milipuko hiyo.

No comments: