Friday, November 1, 2013

MADIWANI WAPINGA TOZO YA FAINI YA SH.LAKI TATU


Na.Edson Raymond
Baadhi ya madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Ikungi mkoani Singida wamepinga sheria ndogo iliyopendekezwa na halmashauri hiyo ya kutoza faini shilingi laki tatu na kifungo cha miezi 12  jela kwa mzazi au mlezi atakayeshindwa kuchangia chakula shuleni.

 
Hatua hiyo imejiri jana katika baraza la madiwani la halmshauri ya wilaya ya Ikungi lililofanyika jana katika ukumbi wa halsmashauri manispaa ya Singida.

 
Mbuge wa Singida Mashariki Tundu Lisu kupitia (CHADEMA) amesema sheria itaibua mgogoro baina ya wananchi kwa kuwa hali ya chakula katika kaya za wilaya hiyo ni ngumu, hivyo akapendekeza sheria hiyo kufutwa.

 

Naye Mbunge Singida Magharibi Muhamed Misanga (CCM) hatua hiyo ni nzuri kwa kuwa inalenga wanafunzi kupata chakula shuleni lakini kunahaja ya kuangalia adhabu hiyo kwani licha ya kutaka kuwekwa kwa msisitizo wa upatikanaji wa chakula hicho, sheria hiyo itasababisha wananchi kuichukia serikali yao

No comments: