Tuesday, November 5, 2013

SHERIA YA DAWA ZA KULEVYA KUWA NA MAHAKAMA MAALUM.


 Na.Iman Musigwa
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Ester Bulaya, ameitaka serikali kufanya mabadiliko ya sheria ya dawa za kulevya na kuanzisha mahakama maalumu ya kushughulikia wahalifu wa dawa hizo

 Amewaslisha maelezo hayo jana kuhusu tatizo sugu la uagizaji, uuzaji na usafirishaji wa dawa hizo ambalo linaloongezeka kwa kasi nchini
Amesema ni wakati mwafaka kwa Bunge na serikali kuona uzito wa tatizo la dawa za kulevya kutokana na ukweli kwamba katika miaka ya karibuni tatizo hilo limeongezeka kwa kasi kubwa hali inayosababisha athari kubwa za kiuchumi
Ripoti mpya ya hivi karibuni ya ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kupambana na Mihadarati na Uhalifu imetamka kwamba Tanzania ni kinara wa kupitisha dawa hizo katika nchi za Afrika Mashariki, na Mkoa wa Tanga kama wa hatari zaidi.

Hata hivyo waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu sera na uratibu wa bunge Bw Wiliamu Lukuvi amesema kauli ya serikali itatolewa kupitia waziri wa katiba  na sheria kuhusu  mikakati ya kutekeleza jambo hilo

No comments: