Wednesday, November 6, 2013

EAC YATARAJIA KUANZA MAZUNGUMZO RASMI NA SUDAN KUSINI








Na.Mwandishi wetu
Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), inatarajia kuanza mazungumzo na Serikali ya Sudan Kusini yatakayohusisha timu ya ngazi ya juu ya wajumbe watatu kutoka nchi wanachama kuhusu ombi la Sudan la kujiunga na EAC.

Katibu Mkuu wa jumuiya ya Africa mashariki Dk. Richard Sezibera, amesema mazungumzo hayo yatakayohusisha timu ya ngazi ya juu yanatarajiwa kufanyika Alhamisi na Ijumaa wiki hii  katika makao makuu ya jumuiya hiyo jijini Arusha

Amesema mazungumzo hayo yanafuatia kikao cha 27 cha Baraza la Mawaziri la Jumuiya hiyo kilichofanyika Agosti 31 mwaka huu, ambacho kiliidhinisha kufanyika mchakato wa mazungumzo na Sudan Kusini kujiunga na EAC

Mazungumzo hayo yanatarajiwa kuwa katika mifumo mitatu ambayo yatahusisha watalaamu kutoka nchi wanachama na awamu ya pili yatahusu makatibu wakuu watakaopitia mapendekezo yaliyotolewa na timu ya wataalam na kuiwasilisha kwenye vikao vya mawaziri na awamu ya tatu itahusu ngazi ya mawaziri.

No comments: