Friday, November 1, 2013

WAZIRI NAHODHA AONGOZA KUTOA HESHMA KWA MAREHEM LUTEN RAJAB MALIMA


Na.Iman Musigwa
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha jana amewaongoza maofisa wa JWTZ katika kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa Luteni Rajab Ahmed Mlima.

Luteni Mlima, aliuawa akiwa na wanagambo wa Kundi la waasi wa M23, katika Milima ya Gavana, karibu na Goma, chini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, wakati akitekeleza jukumu la ulinzi wa amani.

Viongozi wengine walioshiriki katika kutoa heshima zao za mwisho kwa ofisa huyo, ni pamoja na Mnadhimu mkuu wa JWTZ Luteni Jenerali Samuel Albert Ndomba na viongozi mbalimbali wa Serikali

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kutoa heshima hizo, Waziri Nahodha amesema taifa limepoteza mtu shujaa aliyekuwa akitetea roho za watu.

Amesema Serikali haitarudi nyuma katika masuala ya ulinzi wa amani, na kwamba itaendelea kutoa msaada wa ulinzi katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo hadi hapo amani itakapopatikana.

No comments: