Friday, November 1, 2013

UJANGIRI WATISHIA UHAI WA TEMBO NCHINI


Na.Imani Musigwa
Waziri wa  maliasili na utalii balozi khamis Kaghasheki ameliambia bunge  leo mjini Dodoma kuwa ujangiri unatishia uhai wa tembo nchini na kwamba tembo wako katika hatari ya kutoweka endapo hali hiyo haitadhibitiwa

 Kagasheki amesema hayo wakati akitoa tamko bungeni baada ya wabunge Khamisi Mkubwa na Kange Lugora kuomba bunge kuahilisha shuguli zake  ili kujadili ya masuala ya dharula na muhimu kwa taifa ambao ni mgogoro kati ya wafugaji na wakulima

Balozi Kagasheki amesema idadi ya tembo inashuka hali ambayo imeilazimu serikali kuanzisha oparation tokomeza ili kuokoa tembo wasipotee kabisa

 Spika wa bunge Anne Makinda alitoa fursa kwa waziri wa wizara husika  kujibu hoja  ambapo alianza waziri kagasheki na hatimaye waziri wa mifugo na uvuvu Bw mathayo Devid Mathayo

No comments: