Wednesday, November 7, 2012

WIZI WA ALAMA ZA BARABARANI NI KIKWAZO CHA MAENDELEO

 
Na, Doris Meghji Jumatatu

Singida

Uzidishaji wa uzito wa mizigo kwenye magari barabarani,Uwizi wa alama za barabarani, umwagaji oili, Mafuta ya dizeli na Petroli kwenye barabara za lami ni miongoni mwa changamoto zinazoikabili sekta barabara nchini kutodumu kwa muda mrefu wakati serikali inatumia fedha nyingi katika ujenzi wa barabara hizo nchini

Changamoto hizo zimetolewa na Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania DKT.Jakaya Mrisho Kikwete katika ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani singida kwenye uzinduzi wa kukamilika kwa barabara ya Mayoni Issuna mkoani Singida yenye urefu wa kilomita 54 kwa fedha za serikali ya Tanzania kwa gharama ya shilling billion 32 kwa kiwango cha lami yenye kuuganinisha Manyoni na mkoa wa Singida kwa barabara ya lami kuwataka wananchi kutuza barabara hizo ili ziweze kudumu kwa muda mrefu kwa kuwa ndio mishipa ya damu ya uchumi na maendeleo ya wananchi wa Tanzania.

Dkt. Kikwete amesema kukamilika kwa barabra hiyo kumeondolea aibu kwa nchi ya Tanzania kwa watanzania wa wanaokwenda mikoa ya Mwanza na Kagera kulazimika kupita nchi jirani ili kuweza kufika katika mikoa na kipande hicho cha manyoni Isuna kuwa kipande korofi kwa magari kukwama kwa kukwamisha maendeleo ya chni yetu

Naye Dkt John Pombe Magufuli waziri wa ujenzi amesema kukamilka kwa barabara hiyo ni ukombozi mkubwa kwa uchumi wa wananchi wa wilaya ya manyoni na mkoa wa singida kwa ujumla kwa kuwa sasa magari mengi kupita hapo kwa kufanya biashara zao kwenye magari yanayokwenda nchi jirani za Rwanda, Burundi na Uganda kupita katika barabara hiyo mkoani Singida.

Aidha Dr. Magufuli amewataka wananchi kuzingatia sheria namba sita ya barabara kwa kuwa hifadhi ya barabara ni mita 30 na wale waliokwisha lipwa fiadia na kurudi kujenga katika eneo la hifadhi ya barabara kubomolewa nyumba zao bila kulipwa fidia yeyete katika kipande cha kilomita nne kinachoingia mjini Manyoni.

Mkoa wa singida una jumla kilomita 1998 za mtandao wa barabara kati ya kilomita hizo kilomita 357 zimejengwa kwa kiwango cha lami katika ndani cha kipindi cha miaka saba.

No comments: