Saturday, November 24, 2012

UTPC YATOA VIFAA KWA PRESS CLUBS TANZANIA


Muungano wa vilabu vya waandishi wa habari Tanzania umetoa vifaa vya kazi (vitendea kazi) vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 35 kwa kila klabu ya wanahabari kwa lengo la kuboresha utendaji kazi, weledi na kujenga uchumi wa vilabu hivyo

Akikabidhi vifaa hivyo kwa klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Kigoma, vifaa ambavyo ni pamoja na kamera, computer, runinga na zana za kisasa za mikutano na semina (projector), Rais wa UTPC Bw. Kenny Simbaya amehimiza utunzaji wa zana hizo pamoja na nidhamu ya matumizi
Bw. Kenny Simbaya Rais wa UTPC

Bw. Simbaya ameeleza kuwa zana hizo ni matokeo ya utekelezaji wa mradi wa kuimarisha Press Club nchini, mpango ambao umefadhiliwa na mradi wa maendeleo wa Ubalozi wa Sweeden Tanzania
Baadhi ya waandishi wa habari wa Klabu ya Waandishi wa habari mkoani Kigoma wakiwa katika mkutano mkuu maalumu wa marekebisho ya Katiba yao, mkutano huo ulihudhuriwa na pia na Rais wa UTPC Bw. Kenny Simbaya ambaye pia alikabidhi zana za kazi

Tanzania ina jumla ya Vilabu vya waandishi wa habari 23 hadi sasa na upo uwezekano wa kuongezeka kufuatia serikali kuongeza idadi ya mikoa nchini

No comments: