Wednesday, November 21, 2012

SINGIDA PRESS CLUB YAPATA VIFAA VIPYA


 Na Evarista Lucas

Singida 

Nov 21,2012  

Klabu ya Waandishi wa Habari Singida(SINGPRESS) mapema wiki hii imepokea vifaa vya  ofisi vyenye thamani ya shilingi milioni thelathini na tano kwa ajili ya matumizi ya ofisi na ikiwa utekelezaji wa mpango mkakati wa Muungano wa Klabu  za Waandishi wa Habari Tanzania(UTPC).

Akikabidhi vifaa hivyo  mapema wiki hii kwa uongozi wa SINGPRESS; Afisa Programu, mahusiano ya Klabu na ufuatiliaji; Bwana Victor Maleko alisema; “Vifaa hivi tulivyoleta  ni kwaajili ya kuziwezesha Klabu za Waandishi wa habari nchini kuweza kujiendesha zenyewe kwa kutumia vifaa hivi ambavyo vitakuwa kama chanzo cha mapato ya Klabu. Pia ni utekelezaji wa mpango mkakati waUTPC na mkataba uliotiwa  saini na Klabu wanachama ikiwemo mafunzo yanayoendelea kutolewa na UTPC.”

Wakielezea kufarijika kwao na kupatiwa vifaa hivyo; baadhi ya viongozi wa SINGPRESS wamesema kuwa hiyo ni hatua moja kubwa sana kwa Klabu na wanachama wa SINGPRESS kwa ujumla. “ Tutapata na kuongeza kipato  cha Klabu kupitia mmradi wa huduma ya steshenari na ukodishaji wa vifaa mbali mbali vya Klabu kama kamera na vinasa sauti hata projekta.” Alisema kaimu katibu Mtendaji wa SINGPRESS Bwana Elisante John.

 Baadhi ya Vifaa vilivyopokelewa katika ofisi ya SINGPRESS ni pamoja na kamera ya picha za mnato, vidadavuzi, projekta, kinasa sauti, mashine ya  kutolea kopi, video(TV Flat Screen) deki ya DvD ,na  mashine ya kuchomea (laminator) vyenye thamani ya shilingi milioni thelathini na tano tu.

Kwa upande mwingine licha ya kupata vifaa hivyo ambavyo vitawasaidia katika utendaji kazi wao wa kila siku; wanachama wa SINGPRESS wamekuwa wakinufaika na mafunzo mbali mbali yanayoendelea kutolewa na MUungano wa Klabu za Waandishi wa Habri Tanzania ikiwa ni utekelezaji wa mpango mkakati na hati ya makubaliano baina ya UTPC na SINGPRESS uliotiwa saini mnamo mwaka jana.

 

2 comments:

Anonymous said...

Try to edit the story before publish.

STANDARD RADIO FM SINGIDA TANZANIA said...

thank you very much for visiting our bolog and we are happy to receive and publish your online comment. we promise to use it