Tuesday, November 20, 2012

POLISI KUUA MAJAMBAZI NI KUKOMESHA UHARIFU?



Edson Raymond

MWANZA.

Usiku wa kuamkia Nov 14, 2012, kuliripotiwa kuuwawa kwa majambazi wawili kwa kupigwa risasi na askari polisi kwa kile kilichodaiwa kutaka kuhusika kwenye tukio la ujambazi eneo la kilimahewa (big Bite) jiji Mwanza.

Kuuwawa kwa watu hao  ni mwendelezo wa kazi  zinazofanywa na jeshi la polisi jijini mwanza kupambana na uharifu sambamba na kutokomeza mtandao wa majambazi na hadi sasa takribani watu wanane wanaodaiwa kuwa ni majambazi wameuwawa na polisi.

Kutokana na mfululizo wa matukio hayo, nimeanza kupata wasiwasi juu ya uwezo wa jeshi letu la polisi kukabiliana na ujambazi unaoonekana kushika kasi sio mwanza tu bali hata sehemu kubwa ya nchi yetu.

Nimekuwa nikijiuliza kwamba kwa mtindo huu wa kuwauwa majambazi tutamaliza mtandao wao?. Hivi polisi hawana njia madhubuti/mbadala ya kuwakamata majambazi wakiwa hai paosipo kuwauwa?

Nauliza hivyo kwa kuzingatia umuhimu wa kuwakamata majambazi wakiwa hai, ili kujua nani kawatuma, kama tunavyojua kuwa majambazi walio wengi wanakuwa na watu nyuma wanaowawezesha kwa hali na mali maarufu kama wamiliki wa mtandao wa ujambazi, hii ingesaidia kuwahoji na kuufichua mtandao wao badala yake tunaishia kuwauwa?!

Ndiyo tunajua hata hao majambazi  wanakuwa wamejizatiti kama vile kuwa na bunduki za hali ya juu mfano Sub Machine Gun (SMG), lakini polisi ni taasisi kubwa iliyopata mafunzo ya kina ya kukabiliana na adui kwa kila namna pasipo kumuua. Mfano kuna mafunzo ya kulenga shabaha, hivi haiwezekani kutumia ujuzi huo hata kulenga sehemu ambayo itampunguzia makali  jambazi mfano mguu au mkono?

Akiongea na waandishi wa Habari ofisi kwake mrakibu mwandamizi wa jeshi la polisi mkoani Mwanza SSP Lily Matola, alisema kuwa tukio hilo la big bite polisi walikuwa kwenye shughuli zao za kulinda usalama mara wakasikia watu wanawashia risasi ndo hapo na wao wakaanza kujibizana na ndipo wakafanyikiwa kuwauwa watu hao wawili huku watatu wakikimbia!

Kwa kauli hiyo ya Bi: lily kunadhihirisha kuwa polisi wa leo hawahitaji kutumia ujuzi walionao wala kujihangaisha kutumia juhudi zozote za kuhakikisha wanawatia majambazi nguvuni wakiwa hai na badala yake wao wanawauwa tu.

Kwa mtindo huo tutajuaje kuwa hao watu walikuwa ni majambazi? Wametumwa na nani kufanya nini?, wametoka wapi?, na je hao waliokimbia walikimbilia wapi na wamekimbia na nini?

Kumekuwa na malalamiko juu ya askari polisi kuhusishwa na ujambazi! Sasa hisia hizi zitaishaje endapo hao majambazi wasipokamatwa na kuhojiwa na kuwafahamu wahusika wakuu?

Bila jeshi la polisi kuchukua hatua wananchi tusishabikie vitendo vya polisi kuwauwa majambazi pasipo kuwa tia nguvuni wakiwa hai kufanya hivyo watakuwa wanauwawa hawa na wapya wanaibuka kwa sababu wanaowafadhili bado wapo.

No comments: