Saturday, November 10, 2012

SINGIDA WAVUNJA BARABARA KUZUIA AJALI


Na.Khadija. A.Mahamba
Kutoendelea kwetu Tanzania kimiundombinu muda mwingine sisi ndio chanzo cha kurudi nyuma, Hili limedhihirika katika kijiji cha Msisi mkoani Singida pale wananchi walipoamua kuharibu barabara ya lami.
Walichukua maamuzi hayo baada ya mtoto Fazila Silaji kugongwa na gari abiria litokalo Geita kwenda Dar es salaam MJ safari  lenye namba T 729 ASN na kufariki papo hapo.

Sehemu ya barabara iliyoharibiwa na wananchi wa Musisi Singida wakishinikiza wakala wa barabara tanroads kujenga tuta kuepusha ajali kwa watoto wanaovuka barabara hiyo


Hata hivyo jeshi la polisi linaamua kutumia nguvu kuzuia uharibifu huo kwa kutembeza kichapo kwa wananchi ambapo watu kadhaa wanajeruhiwa huku wengine wakipelekwa mahabusu kwa kosa la kujichukulia hatua mkononi

Mmoja wa wananchi waliopata kipigo toka kwa Polisi wa kutuliza ghasia FFU Singida

Wakiongea na Standard Radio wamedai kuwa  kwa muda mrefu wamekua wakiiomba serekali ijenge  matuta katika barabara hiyo kwa kuwa iko karibu na shule ya msingi Msisi  bila mafanikio, hali inayosababisha kutokea ajali mara kwa mara

Wamethibitisha kuwa  katika miezi mitatu iliyopita zimetokea ajali kadhaa zilizosababisha vifo vya takribani  watu watano pamoja na mifungo mbalimbali
Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo kamanda wa vikosi vya usalama barabarani mkoa wa Singida ASP Mohamed Likwata amesema mtoto Fazila Sija mwenye umri wa miaka kumi wa shule ya msingi msisi darasa la nne  amefariki papohapo baada ya kugongwa na basi hilo

Mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoa wa Singida ASP Mohamed akifafanua kuhussu tukio hilo la uvunjivu wa amani na ajali iliyosababisha kifo cha mtoto

Mwili wa marehemu umehifandhiwa katika hospitali ya mkoa wa Singida

Aidha jeshi la polisi mkoani Singida linawashikilia watu kadhaa waliohusika na fujo na uharibifu wa barabara na kwa mujibu wa kamanda Likwata Raia hao wapatao tisa waliodai kuwa na hasira wanafunguliwa mashtaka ya chochea fujo na kuharibu miundo

No comments: