Tuesday, November 20, 2012

MBUNGE AWAPA SOMO WAISLAMU TANZANIA

Na. Halima Jamal
Sinida

WAISLAMU nchini Tanzania, wametakiwa kuongeza kasi zaidi kujikita kumuabudu mungu, ili pamoja na mambo mengine, wasitumiwe ovyo kwenye mambo yasiyokuwa na tija yakiwemo ya maandamano na vurugu.

Hayo yamesemwa na mbunge wa viti maalumu (CCM) mkoani Singida, Martha Mlata, wakati akizungumza kwenye hafla ya harambee ya kuchangia kumalizia ujenzi wa msikiti wa Almasijidi Muhidini Baytulah, wa kitongoji cha Mbuyuni Senene kijiji cha Iguguno, wilayani Mkalama.

Alisema baadhi ya waislamu wamekuwa wakirubuniwa na baadhi ya wanasiasa kuchochea vurugu na wamesahau kuwa wako hapa duniani ili kumuabudu mungu wao na kuwa maisha ya sasa ni magumu hivyo wafanye kazi kwa bidii ili kwa hali hiyo watakuwa wamejijengea mazingira mazuri ya kumudu maisha yao, lakini pia watakuwa na uwezo mpana wa kutambua mema na mabaya.

Mlata alisema kundi kubwa la baadhi ya waislamu hao ni vijana hivyo wakifanya hivyo hawataweza kutumikishwa ovyo ikiwemo kuandamana kwa manufaa ya watu binafsi wanaojitafutia umaarufu, ukiwemo wa kisiasa.

Katika hatu anyingine, mbunge huyo alisema kuwa amani na upendo vinapaswa kuanzia katika ngazi ya kila kaya.

“Kama kwenye familia zetu, hakutakuwepo na amani, upendo na utulivu, basi taifa letu linaweza kuyumba katika juhudi zake za kudumisha amani na utulivu uliopo ambao umedumu kwa muda mrefu sasa”,alifafanua.

Akifafanua zaidi,mbuge huyo,alisema amani na utulivu, vitaendelea kulindwa na kuimarishwa tu, endapo wakazi wa mkoa wa Singida na Watanzania kwa ujumla, watatumia miskiti na makanisa, kumwabudu Mugu kwa uadilifu mkubwa.

Aidha, Mlata alitumia fursa hiyo kuwaasa wazazi walezi kuendelea kuwalea watoto wao katika maadili mema na kuwahimiza watumie nyumba za ibada kwa ajili ya kuwabudu Mungu wao.

Awali Imam wa msikiti wa Nuru Salama Unyankindi Sindia mjini, Yahaya Mahiki, alitumia fursa hiyo kuwataka vijana wa kiislamu na wasio waislamu, kutafuta elimu kwa nguvu zao zote.

Alisema dunia ya sasa, bila elimu ya kutosha, maisha bora kwa kila mtanzania, yatabaki kuwa ndoto.

“Bila kuwa na elimu ya kukidhi mahitaji, wewe kijana utakuwa kama bendera ambayo kazi yake ni kufuata mwelekeo wa upepo. Nenda kwenye maandamano yanayofanyika hivi sasa, utakuwa waandamaji karibu wote ni vijana. Wanashiriki maandamano bila kujua faida zake wala madhara yake”,alisema Mahiki.

Akifafanua zaidi, alisema wanashiriki maandamano kwa vile hawana elimu ya kutosha ya kupambanua jema na baya na yote hayo, yanasababishwa na vijana kutokuwa na elimu.

No comments: