Saturday, November 24, 2012

ALBINO WAOMBA ULINZI ZAIDI TANZANIA


Na  Phesthow  Sanga

Walemavu  wa  ngozi [ALBINO}  Mkoani  Singida  Wameshauriwa  Kujitambua  na Kukubali  hali  Waliyonayo,  kuwa  ni  sawa  na  Watu  Wengine  Wenye  Ngozi  Nyeusi  kote  duniani.

Wito  huo umetolewa na  Ofisa  Ustawi  wa Jamii  Emanuely  Mramba  kwa  niaba  ya  Mkuu  wa  Wilaya  ya  Iramba  Yahya  Nawanda,  katika  Mdahalo  wa chama  cha  maalbino Mkoa wa Singida ,watumishi wa Serikali, Viongozi  wa Dini  na Wadau Wengine  uliofanyika  katika  ukumbi wa Halmashauri ya  wilaya  ya  Iramba.
 

Akisoma Risala kwa  Mgeni  rasmi  katibu  wa Albino  Mkoa wa Singida  Mwanahamisi  Msembo, alisema kuwa  chama  cha Albino  Mkoa wa Singida kilianzishwa  Septemba mwaka 1991 na aliyekuwa  katibu mkuu wa chama hicho marehemu Hamisi maimu kukiwa  na albino  15 tu.
 

Mwanahamisi  alijuza  kuwa  mpaka  sasa  Mkoa  wa  Singida  Unawana chama 338 waliosajiliwa na waliosambaa katika wilaya  zote nne za mkoa wa Singida.

Aidha  Mdahalo huo, ulikuwa Unahoji  kuhusu Ushirikishwaji  wa  watu  wenye Ualbino  katika  shughuli  za  kimaendeleo  ngazi  za  wilaya  mkoani singida,ki-afya ,elimu ,pamoja  na  Ulinzi na Usalama katika  maeneo yote walipo albino kutokanan na vitisho na changamoto  zote zinazowakabili.

Akijibu hoja za Afya kaimu mganga mkuu wa hospitali ya wilaya  Dr.JabirJuma alisema kuwa hospitali yake Imeweka mikakati  dhabiti  ya kupata daktari pamoja  na kilniki ya watu wa Ulemavu wa ngonzi katika  wilaya  ya  Iramba kwa muda  mfupi  ujao .

Hata hivyo kwa  upande wa Elimu ofisa elimu maalum Iramba Bw. Mathew Njoghomi  aliwaeleza  wanamdahalo  kuwa  Idara  yake  inatoa  Elimu  kwa walemavu  wa ngozi {Albino} katika  shule ya Kizega sawa na watoto  wengine  pia wanapewa  Ulinzi wakutosha  wakati wote kutoka kwa jeshi la Polisi pamoja na Jamii

No comments: