Tuesday, September 18, 2012

MATOKEO YA UCHAGUZI CCM ILAMBA


Na.  PHESTHOW  SANGA;

 IRAMBA 

Uchaguzi  wa  Viongozi wa ngazi mbalimbali  katika chama cha  mapinduzi { CCM}Wilayani  Iramba  Mkoani Singida umemalizika juzi sept  8Mwaka huu ,Huku  wanawake  wakiwabwaga  chini vibaya  Wanaume  waliogombea katika  nafasi  za Mwenyekiti .

 

Chaguzi  hizozilizoanza  mapema  Septemba 0 4 Mwaka  huu, kwa  Jumuiya  ya Umoja wa  Wanawake Tanzania { UWT}kwa  Jenephar J. Miano , kufanikiwa kutetea  kiti  chake tena,  baada  ya kutangazwa mshindi  na msimamizi  mkuu  wa uchaguzi huo  { mb} wa singida  magharibi mhe  misanga. kwa  kupata jumla ya kura 334 dhidi ya 48 za  Neema Imaryna 31 za Hawa Rajabu.

 

Aidha kindumbwe-ndumbwe  kilikuwepo  kwenye Jumuiya  mbili  za Umoja wa vijana  CCM pamoja na ya Wazazi, katika Jumuiya  yaVijana  Ambapo  wagombea walikuwa watatukatika nafasi yamwenyekiti , wakiongozwa na Ahamed  Makame ,Athumani Rajabu, pamoja na Mwanamke  pekee  Ziyana J.Mtali.

 

Katika Uchaguzi  huoUliofanyika Spt.08 Mwaka huu  ambapokulikuwa  na Upinzani  kubwa kutokana  na wagombea  wote kuwa na Elimu  nzuri Ingawa Athumani Rajabu ,ni mhitimu wa  chuo kikuu Tumaini Iringa,  lakini hawakuweza kufua  dafu baada  ya kusaliti  Amri kwa Mwana Dada, Ziyana Mtali aliyetangazwa  Mshindi na Msimamizi mkuu  Salumu Mkuya ,kwakupata  kura 187kati ya 275zilizo pigwa.

 

Hata hivyo Mapinduzi ya kuwabwaga  Wanaume yaliendeleakwenye Jumuiya  ya Wazazi, ambapo  huko nako wagombea  walikuwa  watatu kati ya hao Mwanamke alikuwa mmoja  pekee Alisimama kuchuana  na wanaume kugombea  nafasi  ya Mwenyekiti .

 

Katika Uchaguzi  huo  Mwana mama ,Monica Samwely  aliibuka mshindi kwa kupata  jumla ya kura 111.kati ya kura pigwa 237 nakuwapiga  chini  Joseph Kidondela  aliyepata  kura 78 na Selemani  Nyamswa aliyepata jumla ya kura 48.

 

Kwa   nafasi  ya wajumbe wa mkutano  mkuu wa  wataifa, { Uvccm }kulikuwa nawagombea wanne  wawili  walishinda ,kati ya hao ni Amri Said,iMhitimu wa chuo kikuu Tumaini Dsm; na Elilumba Reuben .Wakati katikaJumuiya  ya wazazi walioshinda,ni Alberth  Makwala ,Monica Samwely na Rehema Mkassa,kati ya wagombea sita waliojitokeza kugombea nafasi  hiyo.

 

Katibu wa chama cha mapinduzi{ CCM} Wilaya ya Iramba  bwn , Mathias Shidagisha  Akiongea na waandishiwa Habari Ofisini kwake  leo  Asubuhi alisema  kuwa Uchaguzi  umefanikiwa  kwa Aslimia 95,kutokana  na Wajumbe kuhudhuria kwa wingi  ,Ingawa  kulikuwa  na shida  ya Usafiri mkubwa  sehemu  zingine  kutokana na  jiografia ya wilaya kuwa namabonde pamoja na milima mikali.

 

1 comment:

Anonymous said...

Tunafurahi sana tunapoona habari zianazotolewa na wanahabari wa maeneo husika.Hongereni sana kwa kazi mnayoifanya kwa ajili ya kuwa habarisha Wananchi wa Tanzania.Good work