Thursday, September 27, 2012

MAHAKAMA YAPIGA STOP UCHIMBAJI WA MADINI

NA  Phesthow  Sanga .  Iramba  
Mahakama  Wilayani  Iramba  Mkoani  wa  Singida,Imepiga  marufuku  shughuli  za  Uchimbaji  wa Madini  Ya  dhahabu  katika  Machimbo  ya  Sekenke wilayani  humo  kutokana  na Eneo  hilo kuwa na Mgogoro  Mkubwa   Ambao  Umeshindikana  kusuluhishwa na mkuu wa wilaya  Yahya Nawanda .
Amuri  hiyo  halali Imetolewa  jana  na Hakimu mkuu  Mfawidhi  wa Mahakama hiyo  Mrisho  K.Mrisho Baada  ya kusikiliza  kesi na, 10 ya mwaka 2012 iliyokuwa  inahusu  Zuio la Uchimbaji  Madini,  kati ya Mlalamikaji  John Binner  na   Emmanuel  Magai.
Kwa   Mujibu  wa  hukumu  iliyosomwa  na hakimu huyo  Ilieleza  kuwa, Awali Emmanuel  Magai alipeleka  Ombi  Mahakamani  hapo kuomba  Mahakama  Imzuie John Binner  kujihusisha  na kutaka asilimia 20 ya mapato  ya madini  yanayopatikana  mgodini hapo.
Aidha  ilielezwa  kuwa ,John Binner  naye  alipeleka  Maombi  Mahakamani  hapo  kumzuia  Emmanuel Magai  Kutoendelea  na  Uchimbaji  kwa  Sababu  ameshindwa  kumlipa  Binner  asilimia 20 mwenye  Leseni  halali na mmiliki  wa Mgodi  huo.
Hakimu  Mrisho  alitupilia  mbali Ombi  la Emmanuel  Magai  ,kwa kile alichodai kuwa lilikuwa na Mapungufu ,Alisema  kwa upande wa  John  Binner   vilele kulikuwa  na mapungufu kadhaa  hivyo Mahkama  Inatoa  Amri  ya Mtu yeyote  kutojihusisha  na  Uchimbaji  kuanzia  tarehe  ya kusomwa hukumu  hiyo  jana.
Hakimu huyo  Alisema kuwa,  kwa  kuwa ,Kesi  mama  Inaendelea  katika  Mahakama hiyo,hivyo wote  watulie  Mpaka Mahakama  Itakapotoa  Maamuzi  kuwa  mwenye Uhalali  wa Eneo  hilo ni nani; na hili  Zuio ni la muda  tu.
Kwa  upande wake  Emmanuel  Magai, alisema  kuwa  Yeye ameridhika  na Uamuzi  wa Mahakama kwani  Eneo lililotajwa  ni la kijiji Cha  Mgongo na si Eneo la kijiji Cha   Nkonkilangi   anako fanya kazi yeye.
        Aidha kwa Upande wake  John Binner  naye alisema kuwa ,yeye  ameona   Mahakama  Imetenda  haki iliyopaswa kuitenda  kwa kuwa Tangu amiliki Eneo hilo kihalali  hajawahi  kulipwa  hata shilingi moja na Emmanuel , kama  Walivyokubaliana.

No comments: