Thursday, February 28, 2013

STANDARD RADIO YANG'ARA MTANDAONI

Jumla ya watu 17998 kutoka mataifa kumi na saba duniani wametembelea na kuusoma mtandao wa Standard Radio katika kipindi cha mwezi desemba mwaka 2012 hadi february mwaka huu

kwa Mujibu wa Afisa wetu wa Mawasiliano na chumba cha habari, nchi kinara kwa kusoma na kutembelea mtandao wa Standard Radio ni nchi ya Marekani ambapo watu wapatao 8550 walifungua blog ya www.standardradiofm.blogspot.com na kujisomea habari mbalimbali

Aidha Tanzania inashika nafasi ya pili kwa kuwa na wasomaji 7956 ikifuatiwa na nchi ya Uingereza ambao wasomaji wake wamefikia 527, na kufuatiwa na Urusi, Norway, Ujerumani, Ufaransa, Burundi na Uholanzi.


Picha inaonesha Ramani ya dunia na nchi ambazo zinaongoza kwa kutembelea na kusoma mtandao wa Standard radio iliyoko mkoani Singida nchini Tanzania

Aaidha nchi ambayo ilikuwa na wasomaji wachache ni Kenya, Australia na Bangladesh ambazi wasomaji wake walikuwa chini ya watano

Kwa mujibu wa Mratibu mradi na Meneja wa Radio Bw. Prosper Laurent Kwigize, Kampuni ya Standard Voice LTD inatarajia kuiwezesha radio hiyo kusikika katika mtandao pamoja na satelite hivi karibuni

kusikika kwa radio mtandaoni (internet) kutaongeza idadi zaidi ya wasomaji na wasikilizaji duniani kote.

No comments: