Monday, February 18, 2013

MBUZI AZAA KIUMBE CHENYE MAUMBILE YA BINADAMU

Pichani ni kitoto cha mbuzi chenye sura na maumbile ya binadamu

Mbuzi   mmoja   mali  ya bwana  Iddi Mssoliya   na mke  wake  bi  Rehema  Danford    wakazi  wa kinampanda   wilayani  Iramba    mkoani  hapa   februari  15   mwaka  huu  majira ya   saa moja   Asubuhi   alikutwa   Amezaa  kiumbe   ambacho  kilikuwa  kinafanana  na binadamu  huku  kikiwa  na ngozi  kama  ya  mtu.

 Pichani ni Mbuzi aliyezaa maajabu hayo

Akiongea  na standard  Radio   nyumbani   kwake  jana  bi Rehema , Alieleza  kuwa mbuzi  huyo  ilikuwa  ni   siku  ya tatu   akihangaika  kuzaa  lakini   siku  hiyo alipoamka  limuona  mbuzi  huyo  amezaa na alipoangalia   kilichozaliwa  alishikwa  na  butwaa na   mshangao  mkubwa .
 bi Rehema Danford akiwa nyumbani kwake alishuhudia mbuzi wake akizaa kiumbe cha ajabu

Hata  hivyo   amesema  kuwa , alimweleza  mume   wake   na  wakaenda  kwa afisa  ughani   na kumweleza  habari  hizo  na kwenda  kuangalia  kilichojiri , lakini  afisa  huyo aliwaeleza  wananchi  kuwa  hiyo  ni   hali  ya  kawaida  tu  katika  suala  zima  la  ukuaji  wa  kiumbe katika  mfumo  wa uzazi,

Aidha  Afisa  kilimo  na  mifugo  huyo  Bwn  Aron f. kilazagaye  ametoa  Wito  kwa  Wananchi  wote  kutokuwa  na  Imani potofu  kutokana  na   maajabu  hayo ,  ispokuwa   Watambue  kuwa  hicho  ni  kitu  cha  kawaida  kabisa;  ambacho  kinaweza  kutokea  kutokana   na  ukuaji   wa  kiumbe  kilichomo  katika  mfumo  wa  Uzazi  iwe  ni  binadamu  au mnyama  inaweza  kutokea.

1 comment:

Anonymous said...

Hi! Do you use Twitter? I'd like to follow you if that would be okay. I'm definitely enjoying your blog and look forward to new posts.


Stop by my website :: comprar seguidores en Instagram barato