Friday, February 15, 2013

HABARI ZA KIMATAIFA LEO


NAIROBI

Raia mmoja nchini Kenya ameiomba mahakama kuzuia waangalizi wa uchaguzi kutoka Muungano wa Ulaya kuingia nchini humo kwa lengo hilo kwa madai kuwa wanapendelea baadhi ya wagombea.

Katika kesi iliyowasilishwa mahakamani na mwanaharakati Samson Ojiayo, ameitaka  mahakama kuzuia waangalizi hao kwa Misingi kuwa wanapendelea upande mmoja, huku nchi zao tayari zikiwa zimewaonya wakenya dhidi ya kumpigia kura mgombea Uhuru Kenyatta.

Balozi wa Marekani kuhusu maswala ya Afrika Jonny Carson, amewataka wakenya kufahamu athari za kuchagua baadhi ya wagombea waliojitokeza kuwania urais katika uchaguzi wa Machi tarehe 4.

Mahakama imeelezwa kuwa waangalizi hao tayari wameelezea kutompenda Uhuru Kenyatta na mgombea mwenza wake, William Ruto, kwa kutishia kwa ikiwa wawili hao watashinda uchaguzi huo , wakenya wajiandae kwa athari zake.

Mwanaharakati huyo ameitaka tume huru ya uchaguzi na mipaka, IEBC, kubatilisha idhini ambayo tayari imetolewa kwa waangalizi hao kutoka Marekani, Uingereza na Muungano wa Ulaya ambao tayari wamewasili nchini humo.

Wanapingwa zaidi kwa kupendelea upande mmoja na ikiwa ni hivyo watakuwa wanahujumu misingi ya uhuru na demkokrasia ya Kenya.

Jaji Eric Ogolla, anayesikiliza kesi hiyo atatoa uamuzi Februari 18 mwaka huu.


 

Source:SAPA

Ed: BM

Date: 15 February 2013.

 

 

KINSHASA

 

Zaidi ya wakimbizi elfu nane na mia tano wamekimbia kutoka Jamhuri ya Afrika ya Kati na kuingia katika Jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo wakihofia mashambulizi kutoka kwa waasi wa Seleka.

 

 

Shirika la kuratibu misaada la Umoja wa mataifa OCHA limesema wakimbizi wengi ni watoto, ambao wamepotezana na wazazi wao. Mashirika ya Umoja wa mataifa yameanza kufanya tathimini ya mahitaji ili kutoa misaada kwa wakimbizi hao ambao hadi sasa wanahifadhiwa katika familia za raia katika Jamhuri ya kidemokrasi ya Kongo.

 

Waasi wa kundi la Seleka wanaipinga serikali ya Rais Francois Bozize tangu mwezi Desemba mwaka jana, ingawa viongozi wan chi za Afrika ya kati wamesuluhisha mgogoro na kufikia mkataba wa amani uliosainiwa Januari 11 mjini Libreville nchini Gabon.

 

Chini ya mkataba huo, Waasi wa Seleka waliahidiwa kupewa nyadhifa katika serikali ya Umoja wa kitaifa.  


Source: AFP

Ed: BM

Date: 15 February 2013.

 

SAO PAULO

Shirika la kutetea haki za waandishi wa habari duniani limesema idadi ya waandishi waliofungwa jela katika mazingira yasiyoruhusu uhuru wa vyombo vya habari imepanda mwaka 2012.

 

Shirika hilo Committee to Protect Journalists CPJ  lililo na makao makuu mjini New York nchini Marekani, limesema katika taarifa yake ya mwaka kuwa waandishi wa habari mia mbili thalathini na mbili wamefungwa jela mwaka jana, na kwamba idadi hiyo imepanda tangu lifanye tathimini ya kwanza mwaka 1990.

 

Ripoti ya shirika hilo imesema waandishi wa habari sabini wameuawa wakiwa katika mazingira ya kazi mwaka 2012, ikiwa ni ongezeko la asilimia arobaini na tatu, ikilinganishwa na mwaka 2011.

 

Ripoti hiyo imetaja nchi kumki zilizo katika kiwango cha juu katika mauaji ya  waandishi wa habari kuwa ni Pakistan, Somalia, na Brazil. Nchi nyinine ni Ecuador, Uturuki, Russia, Ethiopia, Vietnam Iran na Syria.

No comments: