Wednesday, February 27, 2013

HABARI KWA UFUPI KUTOKA STANDARD RADIO


*Mkuu wa wilaya ya Iramba mkoani Singida Bw. Yahya Nawanda amewataka wafanyakazi wilayani humo kuacha tabia ya kuwa na vinyongo kazini, na badala yake washirikiane ili kuleta ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao.

Amesema hayo wakati wa uchaguzi wa baraza jipya la wafanyakazi wa halmashauri ya wilaya ya Iramba linaundwa, katika ukumbi  wa mikutano wa halmashauri  hiyo.

 

*Jeshi la Polisi mkoani Singida limekamata bunduki pamoja na mamia ya risasi ambazo zinatajwa kuwa zilikuwa zikisafirishwa kwenda kutekeleza uharifu.

Mkuu wa jeshi la polisi mkoani Singida Kamishna msaidizi wa polisi Linus Sinzumwa mebainisha hayo leo wakati akiongea na Standard Radio

Amesema msako mkali na doria za kina zinafanyika ili kughakikisha waharifu wa aina zote wanatiwa mbaroni

 

*RAIS Paul Kagame wa Rwanda amemteua Mtanzania, Profesa Silas Rwakabamba kuwa Waziri wa Miundombinu wa nchi hiyo katika mabadiliko ya Baraza la Mawaziri yaliyofanyika Jumatatu iliyopita.


Kabla ya uteuzi huo, Profesa Rwakabamba alikuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Taifa cha Rwanda. Ni mmoja wa mawaziri wanaoingiza sura mpya katika Baraza la Rais Kagame ambalo amelifanyia mabadiliko kwa kuunda wizara nyingine mpya.

 

*Kiongozi mkuu wa kanisa katoliki duniani Papa Benedict wa 16 amejiuzulu rasimi leo kama alivyoahidi kufanya mapema mwezi huu

Kabla ya kutekeleza azima hiyo, papa Benedict amefanya misa kubwa katika kanisa kuu la mtakatifu Petro mjini Vatican nchini Italia ambapo maelfu ya waumini walifurika kushuhudia tukio hilo

Papa benedict pamoja na mambo mengine ametoa kauli kuwa anafahamu athari za uamzi wake wa kujiuzuru, lakini amebaki kuwa na amani na imani thabiti kwa Mungu na kanisa lake
 
 

*Zaidi ya watu saba wamefariki dunia baada ya gari moja lililokuwa na bomu kulipuka katika eneo la Kidal nchini mali

Tukio hilo limetokea wakati wanajeshi kutoka nchini Ufaransa wakiwa katika mji wa Kidal nchini mali katika operesheni ya kupambana na wapiganaji wa kiislam tangu mwezi January mwaka huu

 

 

 

 

 

 

No comments: