Friday, February 15, 2013

HABARI ZA TANZANIA


Source: SR/Bandola

Ed: BM

Date: 14 February 2013.

 

SINGIDA

Vijana wametakiwa kutumia fursa zinazowazunguka kwa kujifunza ujasilimali ili kujikomboa kiuchumi

Katibu wa vijana wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Bw. Ibrahim Mluwa amesema hayo katika ofisi za Chama hicho manispaa ya Singida wakati akizungumza na Standard Radio

Bw.Mluwa ameeleza vijana wakiwa makini na waadilifu watakuwa na uwezo wa kubuni mambo ya maendeleo kitendo ambacho kitainua uchumi wa taifa kuliko kuwa tegemezi kama ilivyo sasa.

Aidha Bw. Mluwa amesema CHADEMA imewezesha vikundi mbalimbali na kuvipa elimu ya ujasilimali kitu na kusaidia baadhi ya vijana kujiajiri wenyewe


 

Source: Tanzania Daima

Ed: BM

Date: 14 February 2013.

MOSHI

Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA manispaa ya Moshi kikisema mpango wa mkuu wa mkoa huo wa kutaka kurudisha majimbo yanayoongozwa na upinzani mikononi mwa CCM hauwezi kufanikiwa kwa njia za visasi

CHADEMA kimemtaka Mkuu wa mkoa wa Kilimanajro Bw. Leonidas Gama kuacha kuwagawa wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro na badala yake afanye shughuli za maendeleo zilizompeleka mkoani humo.

Meya wa Manispaa ya Moshi, Bw. Japhary Michael, amesema Gama amekuwa akionyesha upendeleo kwa kuhudhuria mikutano ya CCM huku akitumia mafuta ya serikali jambo ambalo ni kinyume na taratibu

Hata hivyo amesema uchumi wa mkoa huo kwa miaka ya nyuma uliyumba, lakini kwa miaka ya hivi karibu umeanza kupanda kutokana na wawekezaji wengi kuvutiwa na kukubali kuwekeza.


 

Source: Tanzania Daima

Ed: BM

Date: 14 February 2013

SINGIDA

Mwekiti wa taasisi ya SINGIDA ANTS AIDS GROUP Bw Afred Ngoi awametaka wakazi wa mkoa wa Singida kuzingatia mafunzo yanayotolewa juu ya mapambano dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi

Bw Ngoi amesema lengo la taasisi hiyo ni mafunzo kwa wananchi kuhusu  magojwa yanaambukiza kama ukimwi na kuwasaidia waathirika wa ukimwi mahitaji mbalimbali

 

Aidha Bw Ngoi amesema changamoto zinazowakabili ni pamoja  upungufu wa vitendea kazi, uhaba wa watoa mafunzo na uelewa mdogo wa wananchi jambo linalorudisha nyuma maendeleleo ya tasisi hiyo.

 

Naye Bw Sombi Jakson Sombi mmoja wa wanachama wa taasisi hiyo amewataka wananchi kutekeleza elumu wanayopewa na wahudumu wao na kuonyesha ushikiano ili kuepuka majanga yanayoikabili jamii


 

Source: Tanzania Daima

Ed: BM

Date: 14 February 2013

SINGIDA

Mahakama kuu kanda ya kati imewaachia huru washtakiwa Jamali Juma Kuwigwa, Hamza Maagila Simba na Jumaa Msile Zollo wakazi wa Manyoni mjini waliokuwa wameshtakiwa kwa kosa la kuua bila kukusudia

 

Akitoa hukumu ya kesi hiyo jaji wa mahakama kuu kanda ya kati Laurent Kaduri baada ya washtakiwa kusomewa shtaka hilo na kukiri kuwa kitendo hicho kilifanywa na wananchi wenye hasira kali.

 

Chanzo cha kifo hicho kimeelezwa kuwa marehemu Boniphace Kahonga aliiba simu septemba 25-2011 na ndipo washtakiwa walikwenda nyumbani kwa marehemu na kuweza kuondoka nae hadi maeneo ya J.Plazza manyoni mjini.

 

Imeelezwa kuwa walipofika eneo hilo marehemu kahonga alijaribu kuwakimbia na dipo walimita mwizi na wananchi walifika eneo hilo na kuanza kumshmbulia na kumpiga hata kumsababishia majeraha yaliyotoa damu kwa wingi hata kusababisha kifo chake

 

Source: Tanzania Daima

Ed: BM

Date: 14 February 2013.

SINGIDA

Jamii imeshauliwa kutowatenga walemavu wa ngozi na badala yake  iwapende na kuwashirikisha  kwenye shuguli mbalimbali za maendeleo katika jamii

 

Katibu wa chama cha walemavu Tanzania bi Ziada Ally kwenye ulingo wa ushirikishaji  wa shuguli za maendeleo  kwa walemavu  wa ngozi  uliofanyika  katika kata ya  Unyambwa  manispaa ya Singida

 

Mdahalo huo umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wa chama hicho, viongozi wa serikali pamoja na wananchi

Wakizungumza katika mkutano huo baadhi ya wananchi wamesema kuwa walemavu wanapaswa kuheshimiwa  kuthaminiwa kupendwa pamoja na kupatiwa mahitaji mbalimbali yakiwemo kofia za kujikinga na mionzi ya jua na mafuta ya kulainisha ngozi

Hata hivyo wananchi hao wameahidi  kufikisha ujumbe kwa jamii ili kuhusu yale yote waliyoyapata katika  mkutano huo

No comments: