Saturday, February 23, 2013

HABARI FEBRUARY 23, 2013 SR FM


Source: SR/F. Sanga

Ed: BM

Date: 22 February 2013.

 

SINGIDA

 

Mkuu wa mkoa wa Singida Dk. Parseko Kone, jana amemaliza ziara ya siku nne katika wilaya za Iramba na Mkalama, kukagua shughuli za maendeleo ikiwemo kilimo na elimu

 

Katika ziara hiyo ambayo imeanza February 19 wilayani Mkalama, mkuu wa mkoa amekagua ujenzi wa maabara zenye vyumba vitatu kwenye shule za sekondari za kata, kwa ajili ya masomo ya sayansi  ya Biolojia, Kemia, na Fizikia ili ufaulu wa wanafunzi uongezeke kutokana na wanafunzi kufanya mazoezi ya vitendo

 

Dk. Kone amechangia baadhi ya shule ambazo zimefikia hatua nzuri ya ujenzi wa maabara wilayani humo

 

Aidha, Dk. Kone amewataka wakazi wa wilaya hizo kuacha uvivu katika shughuli za kilimo, na kusisitiza walime mazao yanayostahimili ukame kama mtama, muhogo, uwele, viazi vitamu, pamoja na zao la biashara la Alizeti.

 

 


 

Source: SR/O. Samson

Ed: BM

Date: 22 February 2013.

 

IGUNGA

Jeshi la polisi wilayani Igunga mkoani Tabora linamshikilia Bi.Dorothea Zakaria, kwa tuhuma ya kuwaficha wanafunzi 11 wanaosoma darasa la saba katika shule ya msingi Chipukizi iliyopo wilayani humo.

Mmoja wa walezi wa wanafunzi hao Bw. Daniel Winston amesema baada ya kumkosa mdogo wake kwa siku tatu, alifuatilia shuleni na kubaini wanafunzi hao kuishi kwa mtuhumiwa pasipo walimu kujua

Mmoja wa wanafunzi waliofichwa, Masukuzi Mohamed amekiri kuishi kwa mtuhumiwa huyo kwa siku tatu pasipo wazazi kujua na kuongeza kuwa walikuwa wakitishiwa kuuawa endapo watasema wanaishi hapo

Amesema walikuwa wakikesha katika maombezi ya kumwombea mwanafunzi mwenzao Safina Majaliwa, pamoja na wengine waliokuwa wakisumbuliwa na mapepo yaliyokuwa yakiwaangusha mara kwa mara.

 

Mkuu wa polisi wilaya ya Igunga Bw Abeid Maige, amethibitisha kutokea kwa tukio na kufafanua kuwa mtuhumiwa anatarajiwa kufikishwa mahakamani Februari 25 mwaka huu

 

 

Source: SR/E. Chami

Ed: BM

Date: 22 February 2013.

 

SINGIDA

 

Serikali na taasisi mbalimbali mkoani Singida zimeombwa kuangalia wajasiriamali walioko vijijini kwa kuwawekea miundombinu ili kuinua uchumi wa nchi kwa ujumla

Mwezeshaji wa wajasiriamali wadogo wadogo wa shirika la SEDA lilolopo mkoani Singida Bw. Gidion Timoth, amesema wajasiriamali wengi hukimbia vijijini na kwenda mijini wakiamini ndiko penye biashara jambo ambalo si sahihi kwani biashara ni popote.

Amesema hata makampuni mengi ya biashara, benki taasisi zinazotoa mikopo na elimu ya ujasiriamali ziko mjini jambo linalorudisha nyuma maendeleo ya wajasiriamali vijijini.

Amesema ni vyema elimu ikatolewa kwa wajasiriamali walioko vijiini ili kuwajengea mazingira mazuri kwani wengi wao wanapokimbilia mjini hawaendani na mazingira hivyo biashara zao kutoendelea.  

Aidha, amesema kila mtu ana fursa ya kuwa mjasiriamli na suala la ujasiriamali linamkubali kila mtu bila kujali kama ameajiriwa au hajaajiriwa


 

Source: SR/N. LIMU

Ed: BM

Date: 22 February 2013.

 

MTWARA

Mkurugenzi mkuu wa mfuko wa taifa wa bima ya afya NHIF, Bw. Emmanuel Humba, amesema mfuko  umeanza mkakati wa kuboresha usajili wa vitambulisho kwa mfuko wa taifa wa bima ya afya, ili viweze kukidhi mahitaji ya sasa na ya wakati ujao.

Bw  Humba amesema hayo muda mfupi, kabla ya kumkaribisha Naibu waziri wa afya na ustawi wa jamii, Dk. Rashidi Suleimani, kufungua kongamano la wahariri na waandishi wa habari

 Amesema tayari wamekubaliana na shirika la NIDA katika kufanikisha utengenezaji wa vitambulisho hivyo vipya kwa wanachama wa mfuko wa taifa wa bima ya afya.

 Aidha, amesema kuwa lengo kuu la mfuko wa bima kuanzia sasa, ni kuhakikisha watanzania wote wanajiunga na mfuko wa taifa wa bima ya afya na ule mfuko wa afya ya jamii CHF.


 

Source: SR/Lyatuu

Ed: BM

Date: 22 February 2013.

 

SINGIDA

Wananchi mkoani singida wameitaka serikali kuboresha taaluma kwa kuongeza vifaa vya kufundishia ili kuongeza kiwango cha ufaulu wa wanafunzi wa shule za sekondari

 

Hayo yamesemwa na baadhi ya wananchi hao Bw. Shira Saimon mkazi wa Singida wakati akizungumza na standard redio kuhusiana na kutangazwa kwa matokeo mabaya ya kidato cha nne kwa wahitimu wa mwaka jana.

 

Bw. Shira amesema kuwa kufeli kwa wanafunzi wa kidato cha nne ni kutokana na kutokuwepo na vifaa vya kufundishia ikiwemo uhaba wa vitabu, kukosa maabara pia wazazi kutofuatilia maendeleo ya watoto wao kitaaluma

 

Vilevile  kwa upande mwingine amewataka wanafunzi kuwa makini kwa  kutotegemea  vipindi vya darasani na badala yake  wajitume na kujishugulisha kusoma kwa bidii.

 

 Sambamba na hayo naye Bw Tobias Mbaga ambaye pia ni mkazi wa singida amemaliza kwa kusema serikali iandae tume kuu ya usimamizi wa taaluma ili kuboresha elimu

1 comment:

Anonymous said...

Hello my family member! I want to say that this post is awesome, nice written and come with approximately all significant infos.
I'd like to look more posts like this .

Feel free to visit my web site :: marketbookmark.com