Thursday, March 28, 2013

TAARIFA YA HABARI KUTOKA STANDARD RADIO


Source; SR/ Neema J

Ed;

Date; March, 27, 2013

 

SINGIDA

Mkuu wa wilaya ya singida  Bi Queen Mlozi,  amelita jeshi la polisi  kutumia mafunzo watayoyapata  ipasavyo,  na kusema yatawasaidia kuongeza maarifa mapya  na kuleta  mabadiliko,  kwa kuwajibika  katika utendaji kazi wao.

Akizungumza katika uzinduzi wa mafunzo ya jeshi polisi kazini jana Bi Mlozi amesema, maendeleo hayawezi kuja bila changamoto, hivyo  kuwataka polisi  kuhamasishana  katika utendaji kazi wao,   bila kukata tamaa kwani elimu haina mwisho.

Kwa upande wake kamanda wa polisi mkoa wa Singida ACP Linus Sinzumwa, amesema lengo la mafunzo hayo  kutawezesha  afisa  askari  na polisi  ufanisi wa kufanya kazi,  kuleta mabadiliko katika utendaji  kazi wao,  pamoja na kuliwezesha jeshi la polisi kufanya kazi kwa  ufanisi, usasa,  uweledi  pamoja kushirikishaisha jamii, juu ya ulinzi  wa mali zao.

Naye mkufunzi wa   elimu ya watu wazima mkoa wa singida Bw Musa Nkungu,  ambaye ni mmoja  kati ya  watoa mafunzo  kwa jeshi la polisi,  amesema  mafunzo hayo yatawasaidia polisi kupata mafaniko,  ikiwa ni pamoja na  muhitimu   kutunikiwa cheti atakapo hitimu  mafunzo kazini,  na kupandishwa cheo  na kuongezewa madaraka  ya uongozi, katika jeshi la polisi  hivyo kuwataka polisi kuhudhuria katika mafunzo, ili waongeze ufanisi wa kazi .

 

Source; Tanzania Daima

Ed;

Date; March, 27, 2013

DAR ES SALAAM

Serikali imesema haitamvumilia mtu atakayeendesha shughuli za kibinadamu, katika maeneo tengefu  lengo ni kunusuru ikolojia ya Hifadhi za Serengeti, Ngorongoro na Loliondo.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Waziri wa Maliasili na Utalii, Balozi Khamis Kagasheki, amesema wananchi walioingia ndani ya pori tengefu la Loliondo, wanatakiwa kuondoka mara moja.

Balozi Khagasheki amesema kutokana na mgogoro ulioko Loliondo kwa muda mrefu sasa, serikali imepata ufumbuzi ambapo wananchi wanatakiwa kutii sheria bila kushurutishwa.

Aidha amesema ili, kutatua migogoro iliyopo serikali itatenga na kuchukua sehemu ya ardhi ya Pori Tengefu la Loliondo, yenye ukubwa wa kilomita za mraba 1500 kutoka kwenye eneo la kilomita za mraba 4000, za pori hilo.

Source; SR/ Elizabeth, Martine

Ed;

Date; March, 27, 2013

 

SINGIDA

Wanachama wa chama cha walemavu wasiioona mkoani Singida TLB, wanakabiliwa na changamoto mbalimbali katika maisha yao ya kila siku, na kusababisha kushindwa kutekekeleza majukumu yao.

Akizungumza na standard radio mwenyekiti wa chama cha walemavu wa kutoona mkoani singida Bw. Hassani kingugu , ambaye pia ni mlemavu wa kutoona amesema kuwa, changamoto zimekuwa ni tatizo katika maisha yao jambo linalopelekea wao kushindwa kumudu maisha, na kubaki wanahangaika.

Bw. Kingugu amezitaja changamoto hizo kuwa  ni jamii kuwa na mtazamo hasi kwa kudhani walemavu hawawezi kitu, uhaba wa shule, vifaa vya kujifunzia na kufundishia, kubadilika kwa mitaala, kutoshirikishwa kwenye shughuli za ujasiriamali, pamoja na viongozi mbalimbali kutowaelimisha wanajamii, namna ya kuwajali na kuwahudumia walemavu wasioona.

Aidha ametoa wito kwa jamii kutowabagua walemavu na badala yake itambue mchango wao katika maisha ya kila siku, kwani kuna walimu ,wafanyabiashara, mahakimu ambao ni walemavu.

Source; Tanzania Daima

Ed;

Date; March, 27, 2013

TANGA

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Luteni mstaafu Chiku Galawa, amesema tatizo la vijana wengi kukosa ajira linaweza kumalizika ikiwa watavitumia vyuo vya ufundi stadi (VETA), vilivyopo katika maeneo yao.

Mkuu huyo wa mkoa ametoa kauli hiyo katika ziara yake ya kutembelea chuo cha Veta cha jijini Tanga, kwa lengo la kujua hatma ya vijana hao, kupatiwa nafasi mbalimbali, ili hatimaye waondokane na tabia ya kurandaranda mitaani.

Galawa ametumia fursa hiyo kuwataka vijana kutambua fursa hiyo, akiwahakikishia kwamba wanaweza kujikwamua na suala la umaskini, linalowakabili vijana wengi, kutokana na kukosa shughuli za kufanya.
Naye Mkurugenzi wa Chuo cha Ufundi Veta Tanga, Alphonce Kibasha, amemwambia mkuu wa mkoa kwamba changamoto inayowakabili ni uhaba wa majengo, ya kuweza kuchukua vijana wengi kwa wakati mmoja.

No comments: