Thursday, April 25, 2013

CHANJO KWA WATOTO MKOANI SINGIDA

Na. Elisante John, Singida
 
WATOTO 997 Mkoani Singida wenye umri wa chini ya mwaka mmoja, wanatarajia kupata chanjo wakati wa wiki ya chanjo kitaifa, inayoendelea kufanyika nchini kote.

Hayo yamebainishwa na Mganga mkuu Mkoa wa Singida, Dk.Dorothy Kijugu na kubainisha kuwa jumla ya vituo 178 vitatumika kwa ajili ya kufanikisha zoezi hilo, lililoanza juzi Aprili 22 hadi 28, mwaka huu.



Naye mgeni rasmi katika uzinduzi huo uliofanyika leo kwenye kituo cha afya Sokoine Mjini Singida, Mwalimu Queen Mlozi amesifu jitihada zinazofanywa na wauguzi hadi kufikia mkoa kushika nafasi ya kwanza mwaka jana juu ya zoezi hilo na akawataka mwaka huu ushike nafasi ya kwanza.
Katika uzinduzi huo, Dk. Kijugu amesema kwa mujibu wa takwimu za shirika la afya Duniani (WHO) chanjo hizo kwa watoto chini ya mwaka mmoja zinazuia vifo takribani milioni mbili hadi tatu kila mwaka.

No comments: