Thursday, April 25, 2013

VIJANA WAPEWA SOMO-MATUMIZI YA VIDHIBITI MIMBA


Source: SR/Monica

Ed: BM

Date: 25 April 2013.

 SINGIDA

Vijana wametakiwa kutojihusisha na matumizi ya vidhibiti mimba pasipo kujua madhara yake.

Hayo yamesemwa na Bi Judith Kattani mratibu wa Pro-life Tanzania jimbo la Singida na Kahama, alipokuwa akizungumza katika kipindi cha Hoja ya leo jana kinachotangazwa na Standard Radio.

Amesema kuwa vijana wengi wanaathirika na madawa hayo pasipo kujua kutokana na kukosa elimu ya kutosha.

 Bi Judith amesema kutokana na matumizi hayo ya vidhibiti mimba yanachangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa vijana kutokana na kuendekeza mapenzi na kujisahau katika utekelezaji wa majukumu yao.

 Mratibu huyo wa Pro-life Tanzania Bi Judith Kattani ametoa wito pia kwa wanafunzi kutojihusisha na vitendo vya mapenzi wakati wa masomo, jambo ambalo linachangia kwa kiasi kikubwa kushuka kwa kiwango cha elimu kutokana na matumizi hayo ya vidhibiti mimba yanayowafanya kujiamini kuwa hawawezi kupata mimba, jambo ambalo ni hatari kwao kwani huzuia mimba na kusahau kuwa kuna gonjwa la ukimwi.

 Aidha Bi Judith amewaasa wazazi kutoa ushirikiano kwa walimu ili kushirikiana kwa pamoja kuweza kuwalea watoto ili kukuza maadili ya vijana, kwani bila kufanya hivyo kiwango cha elimu kitazidi kushuka na maambukizi ya virisi vya ukimwi yatazidi kuongezeka.

No comments: