Tuesday, March 5, 2013

HABARI KUTOKA STANDARD RADIO


MANYONI

Waziri Mkuu Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania Bw Mizengo Peter Pinda Leo Amezindua Rasim Siku Ya Maadhimisho Ya Siku Ya Utundikaji Mizinga Ili Mananchi Wapate Elimu Ya Ufugaji Nyuki Katika Kijiji Cha Agondi Wilayani Manyoni

 

Hayo yamesemwa na waziri mkuu wa jamuhuri ya muungano wa tanzania katika ziara ya maadhimisho ya kitaifa ya siku ya utundikaji mizinga wilayani manyoni katika mkoa wa singida.

Katika uzinduzi huo pinda amesema zao la asali limetajwa katika vitabu vitakatifu kama bibilia na quruan na kwamba asali ni dawa kutokana na virutubisho vyake bali pia ni chakula.

Aidha pinda amezungumzia kuhusu mikakati iliyopo kutoka wizarani kwamba serikali imeongeza udahili wa wanafunzi katika chuo cha nyuki cha tabora  kutokia wanafunzi 98 hadi kufikia 120 katika chuo hicho.

Katika ziara hiyo waziri mkuu amefwatana na baadhi ya viongozi wa serikali ambao ni waziri wa uwekezaji,kutoka ofisi ya waziri mkuu bi merry nagu na wakuu wa mikoa jirani ya arusha, dodoma na simiyu.

 

 

TABORA

Mchakato wa uundwaji wa mamlaka ya mji mdogo wa Sikonge uko mbioni kukamilika baada ya kamati ndogo iliyoundwa kuwa katika hatua za mwisho.

Akisoma taarifa yake mbele ya Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge mwishoni mwa wiki, mwanasheria wa halmashauri hiyo, Richard Unambwe, amesema tayari kamati yake ilifanya ziara ya kujifunza katika mikoa ya Mbeya na Iringa.

Unambwe ameongeza kuwa mamlaka ya mji mdogo wa Sikonge kwa taratibu zilivyo,  utahusisha vijiji vya Sikonge, Mlogolo, Mwamayunga, Kisanga, Mkolye na Igalula.

Aidha, amesema kuwa hatua nyingine za uanzishwaji zimezingatia uwepo wa ramani inayoonesha mipaka ya mamlaka ya mji husika, maelezo ya utambuzi wa mipaka hiyo kwa kushirikisha vijiji hivyo, ikiwemo ukubwa wa eneo lililotengwa kwa ajili ya kuchukuliwa na mamlaka.

Akihitimisha mjadala huo Unambwe amesema,  hatua nyingine ni kuwepo utayarishaji wa taarifa ya mchanganuo wa matumizi mbalimbali ya ardhi iliyochukuliwa pamoja na vyanzo vya mapato, ikiwemo eneo la makazi, viwanda, taasisi na barabara.

 

 

 

 

DAR ES SALAAM

Rais mtaafu wa Awamu ya Pili, Alhaji Ali Hassan Mwinyi, ameionya jamii ya Kitanzania kuwa makini na watu wanaochochea masuala ya udini.

Mwinyi alitoa wito huo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki katika Ukumbi wa Polisi Mess Msasani, wakati wa uzinduzi wa kipindi cha ‘Pamoja Tunaweza’ kilichobuniwa na Terry Gbemudu maarufu kwa jina la Mama Terry na kuongeza kuwa ni vema kila Mtanzania akajishugulisha na utunzaji wa amani iliyopo, kwani hali ya nchi inakoelekea ni kubaya.

Hata hivyo, ameonya jamii kuwa makini na vurugu za kidini, hasa mauaji ya viongozi wa dini kwani limekuwa suala linalohatarisha amani ya nchi, hivyo ni jukumu la kila mtu kuchukua tahadhari.

Aidha Mwinyi amesema ni vema jukumu la kulea watoto likawa la kila mmoja wetu, kwani hivi sasa kila mtu amekuwa akishughulika na famila yake pekee, jambo ambalo ni hatari kwa siku zijazo kwa watoto wasio kuwa na walezi, wamekuwa hawapati malezi yanayostahili kutoka kwenye jamii.

Kipindi hicho cha televisheni kitakachokuwa kinaelimisha jamii juu ya kupamba na dawa za kulevya, kinatarajiwa kuanza kurushwa na Shikika la Utangazaji Nchini (TBC) kila Jumatatu.

 

 

 

 

SINGIDA

Mwenyekiti wa jumuhiya ya wazazi CCM wilaya ya Ikungi Bw Shabani Hassani Mtakii amewataka watendaji wa vijiji kuwajibika na kuwa na nidhamu katika fedha zinachochangwa na wananchi ili kuepusha migogoro iliyopo kati ya wananchi na serikali kwa kuwasomea wananchi mapato na matumizi ili waweze kujua kupanga vizuri mikakati yao ya maendeleo.

Mtakii ameyasema hayo mwishoni mwa juma katika kijiji cha Mtunduru kata ya Mtunduru wilaya ya Ikungi baada ya kutembelea, kukagua na kuhoji matatizo yaliyosababisha kutomalizika  kwa shule hiyo mpya ya kitongoji cha Mtakuja inayojengwa kwa nguvu za wananchi tangu ianze ujenzi wake mwaka 2000 ambapo hadi sasa ni darasa moja tu limejengwa na ofisi moja ya waalimu huku michango ikitolewa kila mwaka na hakuna maendeleleo ya shule hiyo.

Amesema wananchi wanayo haki ya kudai taarifa za michango yao ya shule inayotumika, na kuhoji taarfa za michango hiyo ilivyotumika na inavyotumika hivyo ni wajibu wa watendaji wa vijiji kuwasomea wananchi taarifa za mapato na matumizi kama katiba inavyoelekeza, ili kuondoa sintofahamu kati ya wananchi na serikali katika fedha wanazochangia miradi.

Kwa upande wake katibu wa jumuiya ya wazazi wilaya ya Ikungi Bw Daud Kapambala amesema lengo la mwenyekiti wa jumuiya hiyo kutembelea shule hiyo ni kukagua, kupokea kero za wananchi na kuhoji matatizo ya kutomalizika kwa shue hiyo      

No comments: