Tuesday, March 19, 2013

DINI NA DOLA HAVIPASWI KUTENGANA KATIKA KUSAKA AMANI NA USALAMA WA TAIFA

Viongozi wa dini wanapoamua kushirikiana na viongozi wa vyombo vya dola ni dhahiri kuwa wameliona na kulitambua tatizo

hapo juu ni Askofu mteule wa jimbo la Bukoba na mlezi wa jimbo katoliki la Singida Askofu Lwoma (kushot) ACP Linus Sinzumwa kamanda wa polisi mkoa wa Singida na Shekhe Salum Ngaa wakiwa katika picha ya pamoja nje ya jengo la matangazo la Standard Radio FM baada ya kushiriki mjadala wa pamoja uliohusu kuwepo kwa dalili, hisia na matukio yanayoashiria udini nchini Tanzania na ushiriki wa vyombo vya dola katika kudhibiti usalama pale inapotokea dini kuanzisha chokochoko zinazotishia usalama wa taifa.

Viongozi wa kiislamu na kikristo mkoani Singida wameunda chombo cha pamoja kitakachoratibu masuala ya amani na usalama, chombo hicho kimepewa jina la kamati ya AMANI NA USALAMA MKONI SINGIDA, hii inaundwa na viongozi wa dini na vyombo vya dola.


Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida Linus Sinzumwa akisalimiana na mwandishi wa habari wa Standard Radio Bw. Boniface Mpagape ambaye pia ni Mhariri wa Habari mara tu baada ya kumalizika kwa mdahalo wa viongozi hao ulioandaliwa na mkuu wa kituo cha Matangazo cha Standard Radio Bw. Prosper Kwigize, kwa lengo la kujadili mstakabali wa amani ya Tanzania na chokochoko za kidini.

1 comment:

Sights & Sounds of Tanzania said...

Ni hatua nzuri sana. Mikutano ya namna hii inahitajika sana, ili kuzuia uchochezwa kuvuruga amani.