Friday, March 1, 2013

SILAHA ZAKAMATWA MKOANI SINGIDA


SINGIDA

Jeshi la polisi na kwa kushirikiana na askari wa misitu wilayani Manyoni Mkoani Singida,  limefanikiwa kukamata zaidi ya  risasi mia mbili na bunduki tatu za magobore.
Kamanda wa Jeshi la polisi mkoani Singida Bw Linus Sinzumwa amesema hay oleo wakati akizungumza na waandishi wa habari, ofisini kwake.

Bw. Sinzumwa amesema kuwa jana majira ya saa kumi na moja asubuhi jeshi la polisi kwa kushirikiana na askari wa misitu wamefanikiwa kukamata risasi na bunduki aina ya magobore katika kijiji cha Sapapa katika tarafa ya Itigi wilayani Manyoni Mkoani Singida. Amesema risasi hizo zinatumika katika bunduki aina ya SMG.

 
Aidha Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani humo ametoa wito kwa raia kutoa taarifa kwa askari ili kuweza kukabilina na vitendo vya kihalifu vinayoendelea kutokea kwani ni njia mbadala ya kukomesha uhalifu.

No comments: