Friday, March 22, 2013

KAMATI YA BUNGE -TAMISEMI YAPATA HOFU SINGIDA


SINGIDA

Kamati ya bunge tawala za mikoa na serikali za mitaa imeitaka serikali kupitia ofisi ya mkaguzi wa hesabu za serikali kufanya uchunguzi wa matumizi mabaya ya fedha zilizotumika kujenga kibanda cha kuchomea taka katika hospitali mpya ya rufaa mkoani Singida.

 

Akitoa maazimio ya kamati hiyo mara baada ya kupokea taarifa fupi kuhusu ujenzi wa hospitali mpya ya rufaa ya mkoa wa singiga leo, Mwenyekiti wa kamati hiyo Dk Hamisi Kigwangara amesema kibanda hicho, kinaonyesha kugharimu milioni 98 na nne jambo ambalo sio sahihi ikilinganishwa na gharama halisi mara baada ya kuona mradi huo.

 

Amesema mkataba wa ujenzi unaonyesha kuwa bati zilizotumika katika ujenzi zinagharimu milioni kumi huku kukiwa hakuna uhalisia kati ya idadi ya bati na fedha iliyotumika jambo linaloonyesha mapungufu

 

Aidha amesema serikali inatakiwa kutuma fedha za kukamilisha mradi wa ujenzi wa hospitali hiyo ambazo zilipitishwa katika bunge takribani bilioni mbili ili kuharakisha ujezi wa hospitali hiyo

 

Kamati hiyo ya bunge imefanya ziara ya siku mbili mkoani Singida ambapo imekagua miradi pamoja na kuzungumza na sekretarieti ya mkoa na imerejea leo mjini Dodoma


Source: SR/Hawa

Ed: BM

Date;21/3/2013

 

SINGIDA

Jumla ya wahamiaji haramu 30 wameripotiwa kuingia mkoani Singida kwa kipindi cha January  2012 hadi march 2013 kinyume cha sheria.

 

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari afisa uhamiaji mkoa wa Singida

Bw.Adam Mnyeke amesema wahamiaji hao wanatoka katika nchi za Ethiopia,Somalia, Burundi na Kenya na kwamba hupita njia zisizo rasmi.

 

Amesema miongoni mwa wahamiaji hao waethiopia ni 24,wasomali 3, wakenya 2 na mrundi mmoja.

 

Aidha amesema uchunguzi umebaini chanzo cha wahamiaji hao haramu kutoka katika nchi zao kuwenda nchi jirani ni  kutokana na hali ngumu ya maisha, na hali mbaya ya kiusalama katika nchi zao,na hufanya hivyo kunusuru maisha yao

 


Source: SR/Bandola

Ed: BM

Date;21/3/2013

 

SINGIDA

Wito umetolewa kwa wananchi kwa kushirikiana na vikundi vya polisi jamii katika suala la kufanya usafi katika kata ya utemini ndani ya manispaa ya Singida

 

Mtendaji wa kata  hiyo Bw. Noel Hago ametoa wito huo wakati akiongea na Standard Redio leo ofisini kwake.

 

Bw. Hago amesema hayo kufuatia siku iliyopangwa na viongozi kwa kushirikiana na  polisi kata, kufanya usafi siku ya tarehe 22 mwezi 3 mwaka huu.

 

Aidha Bw. Hago amesema wananchi wanapaswa kuonyesha ushirikiano wao dhidi ya viongozi ili kuweza kufanikisha zoezi hilo.

 

 

 


Source: SR/Hawa

Ed: BM

Date;21/3/2013

 

SINGIDA

 Chama cha wafanyabiashara, viwanda,na kilimo mkoani singida  TCCIA  kinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upungufu wa fedha na kukosa wafadhili.

 

Hayo yamesemwa na afisa mtendaji wa chama hicho mkoani singida Bw. Calvert Nkurlu wakati akizungumza na standard radio ofisini kwake.

 

Amesema chama hicho kilianzishwa kwa lengo la kuunganisha nguvu ya wafanyabiashara, viwanda, pamoja na wakulima wawe na sauti moja katika masuala yanayowahusu ili kuendesha biashara kwa ufanisi

 

Aidha chama mkoani Singida kina wanachama mia sita themanini na sita, idadi ambayo ni ndogo ikilinganishwa na wafanyabiashara na wakulima waliopo katika mkoa wa singida

 

Ametoa wito kwa wafanya biashara kutumia mitandao mbalimbali ili kupata habari zinazohusu biashara, kusajili majina ya biashara, pamoja serikali kukaa pamoja na wafanyabiasha ili kujadili hali halisi ya biashara
Source: Tanzania Daima

Ed: BM

Date;21/3/2013

 

BUKOBA

Baadhi ya madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba wamedai kuwa Meya wao, Anatory Amani, amekuwa akiendesha shughuli zake kibabe, ikiwa ni pamoja na kuidhinisha matumizi ya fedha bila kuwashirikisha.

Madiwani hao wametoa madai hayo jana mbele ya tume iliyoundwa na Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), kuchunguza tuhuma za ufisadi wa miradi mitatu zinazomkabili meya huyo, ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro.

Wajumbe wengine mbali na Kandoro ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk. Rehema Nchimbi, Naibu Katibu Mkuu wa Tamisemi na Naibu Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

Madiwani hao kwa nyakati tofauti wameiambia tume kuwa Amani amekuwa mbabe na kufikia hatua ya kuhamisha fedha kutoka mfuko wa mradi wa viwanja sh milioni 200 kwenda kulipia deni la mradi wa soko bila idhini yao.
Source: SR/E. Lyatuu

Ed: BM

Date;21/3/2013

SINGIDA

Wananchi wa kijiji cha Mandewa Kata ya Mandewa manispaa ya Singida, wametakiwa kuwa na subira kuhusu suala la kuhamishwa kwa soko la gineri

 

Mtendaji wa Kata hiyo Bw. Bakari Ntandu amesema hayo wakati akizungumza na standard radio ofisini kwake, kuhusu mikakati iliyopo ya kuhamishwa kwa soko hilo.

 

Amesema eneo linalotumika kama soko, linatumika kwa muda na wala halikupangwa maalum kwa ajili ya soko na kwamba lipo eneo husika kwa ajili hiyo na utaratibu wa kuhamia katika eneo hilo unafanyika.

 

Amesema utaratibu unaofanyika ni kusubiri kampuni ya Spencon kukamilisha mradi wa maji, kwa kuwa eneo lililotengwa kwa ajili ya soko lipo karibu na mradi wa maji unaojengwa.

 
Aidha amewataka wananchi kuwa tayari kuhama katika eneo linatumika kama soko, kwa kuwa si eneo lililotengwa maalum kwa ajili ya biashara, kwa kufuata taratibu na kutoeneza uvumi kuhusu kuhamishwa kwa soko

No comments: