Wednesday, December 5, 2012

WAZIRI HIMIZA UZALENDO KATIKA MATANGAZO YA RADIO NA RUNINGA


Waziri wa mawasiliano ysayansi na teknolojia profesa Makame Mbalawa, ametoa wito kwa vyombo vya utangazaji kuepuka kutangaza zaidi muziki na matangazo ya nje ya nchi badala yake vipindi na habari zinazowahusu watanzania zipewe kipaumbele zaidi

Profesa makame amesema hay oleo jijini Dar es salaam wakat akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa watangazaji nchini pamoja na mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA

Amebainisha kuwa, vyomboo vingi vya habari hasa radio na televisheni vimekuwa vikitoa nafasi kubwa ya kutangaza muziki na vipindi vingi kutoka nje ya nchi jambo ambalo linawanyima watanzania kujifunza mambo yanayowahusu

Aidha ametoa wito kwa watangazaji wote Tanzania kuwapa kipaumbele watanzania wa vijijini kwa kuandaa vipindi na matangaza ambayo yatawasaidia kubadilika kimaendeleo kutka walipoo kwa kutumia vyombo vya habari

Hata hivyo profesa Mbalawa ameonya uwepo wa ukiukwaji wa maadili ya utangazaji na kutoa wito kwa watangazaji wote kutumia fursa ya matangazo ya mfumo wa digitali kusimamia vema maadili ya taaluma ya utangazaji.

Tanzania imeazimia kuzima mitambo ya mfumo wa analogia na kuwasha digitali ifikapo desemba 31 mwaka huu kwa mikoa ambayo huduma hiyo inapatikana.

1 comment:

Agnes Shayo said...

Nawaunga mkono wadau wote mnaotuhabarisha kupitia blog hii kwani mnatupa habari moto moto. Naunga mkono wito ambao umetolewana Waziri, ni kweli sisi wadau wa habari hasa Watangazaji kuna mahali tunajisahau kuwa sisi ni SAUTI ya WASIO na SAUTI, kumbe basi wadau tuungane pamoja katika kutekeleza wito wa Waziri kwa lengo la kuikomboa nchi yetu.