Pageviews by Countries
|
Pageviews by Browsers
|
Thursday, May 23, 2013
STANDARD RADIO AUDIENCE- THIS WEEK
BBC YABISHA HODI STANDARD RADIO FM - MCHAKATO WA USHIRIKIANO WAANZA
Na Boniface Mpagape.
Standard Radio FM iliyopo mjini
Singida, imeanza mchakato wa kushirikiana na Shirika la
utangazaji la Uingereza BBC katika kurusha baadhi ya vipindi na matangazo
kutoka shirika hilo.
Hali hiyo imedhihirika baada ya
Shirika la BBC Media Action kutuma afisa utafiti wake Bi. Suzy Matamwa ambaye
kulingana na maelezo yake mbele ya watumishi wa Standard radio atakuwa na
mazungumzo ya ana kwa ana na kila mwandishi kuhusiana na shughuli za kila siku
zinazofanyika katika masuala mbali mbali ya uandaaji wa habari na vipindi mbalimbali.
PIC 1. Bi. Suzy Matama akiwa katika picha ya
pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Standard Radio katika ofisi za SR FM. Kutoka
kulia ni Meneja wa SR Bw. Prosper Kwigize, Mkurugenzi wa SR Bw. James Daud na
Bi. Suzy Matama kutoka BBC Media Action, wakati akitambulishwa rasmi.
Naye meneja wa Standard radio Bw. Prosper Kwigize amesema
kuwa Standard radio inatangaza vipindi mbali mbali vinavyoigusa jamii moja kwa
moja katika nyanja mbali mbali zikiwemo za afya, elimu, kilimo, uchumi, ambavyo
hutangazwa na redio hiyo.
Aidha amesema standard radio imekuwa ikipokea wanafunzi
kutoka vyuo mbali mbali vya uandishi wa habari hapa nchini.
Amesema hivi sasa
kuna wanafunzi wanne waliopo katika mafunzo kazini na kwamba wengine
waliokuwepo wamemaliza muda wao na kurejea kwao na kwamba zaidi ya wanafunzi watango kutoka chuo kikuu cha mtakatifu Augustino cha jijini Mwanza wanatarajia kuanza mafunzo kwa vitendo ndani ya Standard radio hivi karibuni
Afisa utafiti huyo kutoka shirika la BBC Media Action, amesema atakuwa akizungumza na wafanyakazi wa standard radio kwa nyakati tofauti kwa muda wa siku tatu, kuhusu masuala ya kawaida kama uandaaji wa vipindi, habari na kurusha matangazo kwa ujumla.
Endapo mpango huo utafanikiwa
itakuwa ni fursa nzuri kwa wakazi wa Singida kuweza kusikika katika ngazi ya
kimataifa kupitia BBC kwani nao pia watapata fursa ya kuchangia maoni
yao kuhusu masuala mbali mbali katika jamii.
Watumishi wa Standard radio pia
watanufaika kwa kupatiwa mafunzo pamoja na vitendea kazi ili kuwezesha ufanisi
katika kazi za kila siku za kuhabarisha na kuelimisha jamii.
PIC 2. Meneja wa SR FM Bw.
Prosper Kwigize (Katikati) akitambulisha baadhi ya wafanyakazi wa standard
radio kwa mgeni kutoka BBC Media Action.
Kulia kwake ni mtangazaji na mwandaaji wa vipindi Bw. Cales Katemana na
kushoto kwake ni fundi mitambo wa SR Bw. Moses Anthony.
PIC 3. Mtafiti kutoka BBC Media Action Bi. Matama (aliyeinama kulia) akisikiliza kwa makini majina ya wafanyakazi wa SR bali pia kutaka kujua kila mmoja anafananaje, wakati wakitambulisha kwake. Kushoto kwake ni Mkurugenzi wa SR. Bw. James Daud.
Saturday, May 18, 2013
WASOMI KUTOKA KIGOMA WALIA NA WABUNGE WAO
Wabunge wa mkoa wa Kigoma wamehimizwa kujenga umoja na kuwa
na mkakati maalumu wa kuutetea mkoa wa Kigoma na kuepuka ushabiki wa kisiasa
ambao unatajwa kuiangamiza Tanzania
Raia hiyo imetolewa leo mjini Dodoma na Amos Nyandwi (pichani hapo juu) mchumi
kutoka wizara ya kazi na ajira ambaye pia ni mwenyeji wa mkoa wa Kigoma katika
kongamano la vijana wasomi kutoka vyuo mbalimbali nchini ambao ni wazawa wa
Kigoma
Bw. Nyandwi amebainisha kuwa kwa sasa wabunge wote wa majimbo
na viti maalumu kutoka mkoa wa kigoma hawajaonesha
umahili wao katika kubuni na kusimamia mipango ya maendeleo kwa njia ya umoja
kama wawakilishi wa wanakigoma Bungeni
Amesisitiza kuwa licha ya kuwepo na wataalam walioajiliwa
serikalini na katika sekta binafsi ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakisaidia
kuchochea wabunge hao kuungana na kuwatumia wataalamu kuibua na kusimamia
maendeleo lakini hakuna mwitikio wa wabunge hao
Aidha Nyandwi ameonya juu ya wanasiasa kung’ang’ana na vyma
vya siasa na kushindwa kusimamia maslahi ya wananchi ambao ndio waliowapigia
kura
Pamoja na lawama hizo kwa wabunge na wanasiasa, mchumi huyo
amewahimiza wasomi walioko katika vyuo kufikiri kurejea mkoani Kigoma na kuunda
au kujiunga na vikundi vya ujasiriamali ii kunufaika na mipango ya serikali ya
uwezeshaji jamii kiuchumi.
Kwa upande wake mkurugenzi wa makampuni ya Buhanzo na Standard
Voice limited Bw. James Japhet (pichani hapo juu) amewaonya wasomi kutoka Kigoma kuondoa fikra za
kutaka kuajiriwa badala yake wasome kwa umakini na watumie alimu yao kwa ajili
ya ujasiriamali
Bw. Japhet ameongeza kuwa mkoa wa Kigoma una vyanzo vingi vya
uchumi ambavyo havijatumika kuwainua wakazi wa mkkoa wa Kigoma hususani mazao
ya ziwa Tanganyika, kilimo, ufugaji na fursa za biashara katika mipaka ya nchi
jirani za Burundi, DRC na Zambia.
Aidha Bw. Japhet amewataka wabunge wa mkoa wa Kigoma kuungana
pamoja kutetea ujenzi wa barabara pamoja na mkoa kuunganishwa na umeme wa gridi
ya taifa, na kwamba bila miundombinu ya umeme na barabara za uhakika Kigoma
haitapata maendeleo endelevu.
Zaidi ya wanafunzi 80 kutoka vyuo vya SAUT, Udom, SUA,
Mzumbe, St. John, RUAHA na Tumaini wamehudhuria kongamano hilo, ambapo ni mbunge mmoja tu kutoka jimbo la Muhambwe Bw. Felix Mkosamali (pichani aliyekaa katikati juu) aliyejitokeza kushiriki.
Tuesday, May 7, 2013
MAALIM SEIF SHARIF HAMAD AZURU MKOA WA SINGIDA
MAKAMU wa kwanza wa Rais, Serikali ya mapinduzi Zanzibar Seif Sharif Hamadi
amewataka Watanzania kudumisha upendo baina yao ili kuepuka chuki zinazoanza
kujitokeza sasa nchini, kiasi cha kusababisha vurugu na vifo kwa wananchi wasiyo
na hatia.
Alitumia fursa hiyo kuitaka serikali ya Tanzania
kufuatilia kwa makini tukio la ulipuaji bomu katika ibada ya ufunguzi wa kanisa katoliki la Mtakatifu Joseph mkoani Arusha, ili waliohusika
wote wakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Maalimu Seif amesema hayo mjini Singida, kwenye
ziara yake ya siku mbili mkoani humo iliyoanza May 06 2013 ambapo alipokelewa na viongozi wa serikali na chama cha wananchi CUF mkoani humo.
katika hotuba yake Bw. Seif amesema Watanzania siku zote wamekuwa ni watu wa amani,
lakini vurugu zinazoanza kujitokeza sasa siyo za kistaarabu na zinaashiria kuna
watu wanaochochea ili kufanikisha malengo waliyokusudia.
Alitumia fursa hiyo kuitaka serikali ya Tanzania
kufuatilia kwa makini tukio la ulipuaji bomu katika ibada ya ufunguzi wa kanisa katoliki la Mtakatifu Joseph mkoani Arusha, ili waliohusika
wote wakamatwe na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
PICHA: Mkuu wa wilaya ya Singida Mwl. Queen Mlozi akimkaribisha jukwaani Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar ili kumpa fursa ya kuhutubia umati wa wananchi mjini Singida
Aidha alilaani shanbulio hilo la bomu kuiomba Serikali
iendelee kulinda usalama wa wananchi wake kwa ajili ya kuenzi misingi imara ya
amani, umoja na upendo iliyoasisiwa na waazilishi wa Taifa la
Tanzania.
Makamu wa kwanza wa Rais Seif Sharif Hamad alimaliza
ziara yake jana na alitarajiwa kuondoka mkoani Singida ili kuendelea na majukumu
mengine ya kitaifa.
Subscribe to:
Posts (Atom)









