Thursday, October 24, 2013

WAKAZI WA MKOA WA SINGIDA KUDUMISHA USAFI




Na.Anna chiganga
Kamati za mazingira kwenye serikali za mitaa mkoani singida zimetakiwa kuhamasisha wakazi wa mkoa wa singida kudumisha usafi katika maeneo yao kwa lengo la kuboresha manisapaa ya Singida

Akizungumza katika uzinduzi wa kamati za afya na mazingira mkurugenzi wa manspaa ya singida Bw Joseph Mchina amewataka watendaji wa mitaa na kata kuhakikisha manisipaa inakuwa katika mazingira safi na salama.

Amesema kila mtendaji wa kata atapewa lori la kubeba uchafu ili na atakayebainika kutupa taka ovyo awajibike ikiwa ni pamoja na kulipa faini

Aidha amewataka wananchi kuhakikisha wanatupa taka taka katika eneo husika pindi wanapomaliza kutumia mifuko ya Rambo ikiwa ni pamoja na kuichoma

Wednesday, October 23, 2013

MKOA WA SINGIDA WADHIBITI VITENDO VYA UHALIFU






                    MRAKIBU WA POLISI BW.JAMES KASUSURA

Na.Edson Raymond
Mkoa wa Singida ni miongoni mwa mikoa minne nchini iliyofanikiwa kupambana na vitendo vya uhalifu kwa kiwango kikubwa kwa kipindi cha hivi karibuni.

Mrakibu  wa Polisi kutoka makao makuu Dar es salaam kitengo cha maadili James Kasusura amesema hayo wakati akizungumza na washiriki wa kikao cha siku maalum ya polisi kilichofanyika katika ukumbi wa Aquar manispaa ya Singida.

Kasusura ameyataja makosa yaliyopungua kuwa ni makosa dhidi ya ubinadamu ambayo yamepungua kwa asilimia 35, makosa dhidi ya mali yamepungua kwa asilimia 18, makosa dhidi ya maadili yamepungua kwa sailimia 13, na makosa dhidi ya usalama barabarani yamepungua kwa asilimia 12.

Amesema kupungua kwa makosa hayo kumetokana na ushirikiano baina ya raia na vyombo vya ulinzi na usalama mkoani Singida, hivyo kutoa wito wa kuendelezwa kwa ushirikiano huo na hatimae kukomesha vitendo hivyo kabisa.


WAHUKUMIWA MIAKA 30 KWA KUTEKA MAITI





majambazi wakipelekwa magereza baada ya kuteka maiti



Na.Edilitruda chami
Watu wanne wamehukumiwa kifungo cha miaka 30 Jela kwa kosa la unyanganyi wa zaidi ya shilling milioni nane kwa kutumia silaha

Akisoma hukumu hiyo hakimu mfawidhi wa mahakama ya wilaya mkoani Singida Flora Ndale amesema tukio hilo limetokea desember 8 waka 2012 katika barabara ya singida kwenda Dodoma maeno ya kisaki

Amesema siku ya tukio washtakiwa waliweka mawe barabarani na kuteka gari lililokua likisafirisha maiti ya mwanafuzi wa chuo kikuu cha Sokoine {SUA] kutoka morogoro kuelekea Tarime

Katika tukio hilo vitu mbalimbali kama laptop, simu za mkononi, moderm mbili zote vikiwa na thamani ya shilingi milioni nane laki saba viliibwa

Amewataja waliohukumiwa kuwa ni Hamisi Issa, Halidi Hamisi, Abbubakari Jumanne, Hamisi Alli wote wakazi wa mkoa wa Singida,ambapo siku ya tukio walikuwa na rungu,mawe na mashoka wakitumia kufanya uhalifu huo
Hakimu Ndale amesema kitendo hicho ni amesema adhabu hiyo itakua fundisho kwa watu wengine wanaofanya vitendo kama hivyo.

MSAKO MAALUM KWA WANAOISHI KINYUME NA SHERIA MKOANI SINGIDA





 Na.edson raymond

Mkoa wa singida unatarajia kuanza operation ya ukaguzi wa kubaini watu wanaoishi nchini kinyume na sheria.

Hayo yamebainishwa jana na Afisa uhamiaji mkoa wa Singida Bw. Adam Mnyeke wakati akizungumza katika siku maalum ya polisi iliyofanyika katika ukumbi wa Aquar Manispaa ya Singida,

Bw. Mnyeke amesema kuwa zoezi hilo linatarajia kuanza wiki ijayo, hivyo kutoa wito kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa taasisi hiyo ili kupambana na wahamiaji haramu.

Amesema kwa kuanza, zoezi hilo litaanzia manispaa ya singida na baadaye litakwenda katika wilaya nyingine za mkoa wa Singida, na kuongeza kuwa zoezi hilo pia litasaidia kupambana na vitendo vya uhalifu ambavyo mara nyingi vimekuwa vikifanywa na wahamiaji haramu.