Wednesday, June 5, 2013

SANAA NI SEHEMU YA BURUDANI NA AJIRA KWA VIJANA

WANANCHI WAHIMIZWA KUTUMIA VYOMBO VYA HABARI KWA USTAWI WA JAMII



pichani ni viongozi wa serikali ya wilaya ya Iramba pamoja na Meneja wa Standard Radio fm, Bw. Prosper Kwigize (katikati mwenye Kaunda suti) wakiwa katika picha ya pamoja baada ya tamasha la kuitangaza Radio hiyo wilayani Iramba
Wakazi wa wilaya ya Iramba mkoani Singida, wametakiwa kuitumia Standard Radio katika kufikisha ujumbe kwa jamii na kushiriki kikamilifu katika uandaaji wa vipindi vya kuelimisha umma.
Wito huo umetolewa mwishoni mwa wiki na Mkuu wa wilaya ya Iramba Bw. Yahaya Nawanda, katika hotuba yake iliyosomwa na Katibu tawala wa wilaya ya Iramba Bw. Yahya Naniya, wakati wa utambuilisho wa Standard radio kwa wakazi wa wilaya hiyo uliofanyika katika stendi ya mabasi ya mjini Kiomboi.

Katibu tawala wa wilaya ya Iramba Bw. Yahya Nania (mwenye suti na miwani) akijiandaa kutoa hotuba ya mkuu wa wilaya ya Iramba Bw. Yahya Nawanda)
Amesema mawasiliano ni kitu muhimu katika jamii kwani hurahisisha mambo mengi ikiwa ni pamoja na kufikisha ujumbe kwa haraka, lamoja na kuweza kujipatias wateja wengi kutokana na kujitangaza kibiashara.
Awali meneja wa Standard radio Bw. Prosper Kwigize amesema, Standard radio ipo ili kukidhi haja ya wakazi wa mkoa wa Singida kwani ni radio ya kwanza kuanza kutangaza ndani ya mkioa wa Singida tangu kupatikana kwa uhuru wa Tanganyika zaidi ya miaka hamsini iliyopita.
 
Bw. Kwigize amesema msimamo wa Standard radio haugemei upande wowote kidini, kisiasa au kijamii, bali ni radio ambayo inatoa huduma zake kwa wananchi wote bila ubaguzi, na kuwataka wakazi wa wilaya ya Iramba kuitumia ipasavyo.

 

MTOTO MCHANGA ATELEKEZWA NA MAMAE MJINI SINGIDA


Mtoto anaekadiriwa kuwa na umri wa miezi sita ameokotwa akiwa ametupwa katika kitongoji cha unyakumi kata ya mandewa mkoani Singida

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo afisa mtendaji wa kijiji hichi bi.Hadija Msumari amesema mtoto huyo wa jinsia ya kiume  ameokotwa katika nyumba iliyokuwa ikijengwa  ya bwana Sadiki juma.

Amesema baadhi ya vitu alivyokutwa navyo ni pamoja na begi dogo la nguo,chupa ya uji,na kadi ya kliniki


Akifafanua zaidi amesema kadi ya mtoto inaonesha kwa mara ya mwisho alipelekwa katika kliniki ya uhasibu mjini singida na anaishi kitongoji cha misake na mwenyekiti wa eneo hilo ni bwana Hamisi Mdadi huku jina la mtoto na wazazi likiwa limefutwa

Nyumba alimookotwa mtoto alietelekezwa na mama yake

Aidha mmoja wa mashuhuda ambae amemuokota mtoto huyo bi.Hadija  shabani amesema alikuwa akipita jirani na eneo la tukio majira ya saa mbili asubuhi na kumsikia mtoto akilia kwa muda mrefu ndipo bila kuhisi dalili yoyote ya msaada  ndipo alipoamua kuingia ndani na kumkuta mtoto akiwa peke yake

Jeshi la polisi mkoani singida limemchukua mtoto huyo kufanya uchunguzi ili kumbaini anaehusika na tukio hilo la kinyama
 
Imeandikwa na Edilitruda Chami

Thursday, May 23, 2013

DW WATOA UDHAMINI KWA STANDARD RADIO FM- USHIRIKIANO WAANZA


Shirika la utangazaji la Ujerumani DW limetoa vifaa vya mawasiiano na utangazaji kwa Standard Radio FM, kama sehemu ya kujenga ushirikiano wa kihabari baina ya Radio za kimataifa Radio za kijamii barani afrika.

Vifaa hivyo vyenye thamani ya zaidi ya dola za kimarekani 300 vimetolewa mwezi april mwaka huu na standard radio imeanza kuvitumia kuunganisha matangazo ya DW na wasikilizaji wa Standard Radio FM

Sambamba na hayo Standard Radio iliyoko mkoani Singida imetiliana saini ya ushirikiano wa muda mrefu wa kihabari na DW na upo mkakati wa wafanyakazi wa SR fm hususani waandishi wa habari na watangazaji kuanza kupata mafunzo yanayotolewa na kituo cha mafunzo ya kitaaluma cha DW kijulikanacho kama Deutch welle Ackademie

Standard Radio iliyoanza matangazo yake mwezi January mwaka huu imekuwa kwa kasi kufuatia kuwa na mikakati kabambe ya kuhakikisha inakuwa Radio Bora katika eneo la Tanzania na maziwa makuu