Wednesday, January 2, 2013

MILIONI 92 ZAJENGA MAABARA SINGIDA


Zaidi ya shilingi milioni 92.3 zimetumika kugharamia ujenzi wa maabara mbili katika shule ya sekondari ya Ipembe katika manispaa ya Singida mjini hapa.

Mkurugenzi wa manispaa hiyo,Mathias Mwangu aliyasema hayo juzi wakati akizungumzia zoezi la ujenzi wa maabara katika halmashauri hiyo.

Alisema kuwa kati ya fedha hizo, serikali kuu imechangia shilingi 80 milioni na nguvu kazi ya wananchi,imechangia shilingi 12,385,000.

Mwangu alisema wamejenga maabara hizo za biolojia na kemia,ili kuwasaidia wanafunzi kujifunza kwa vitendo masomo ya sayansi.

“Lengo kuu la kujenga maabara haya,ni kuwasaidia wanafunzi kujifunza kwa vitendo masomo ya sayansi,pia kuwafanya wanafunzi kuyapenda masomo ya sayansi na kuongeza kiwango cha ufaulu wao”,alifafanua.

Aidha,mkurugenzi huyo,alisema kuwa maabara hayo yatasaidia pia wanafunzi wa shule jirani zisizo na maabara kufika na kujifunza kwa vitendo masomo ya sayansi hususani kemia na biolojia.

Mwangu alitaja changamoto inayowakabili hivi sasa,ni kuendelea kununua vifaa muhimu vya maabara na pia kuanza ujenzi wa maabara ya fizikia.

Mkuu wa wilaya ya Singida,mwalimu Queen Mlozi,ameagiza kila sekondari ya kata,zihakikishe zinajenga vyumba vitatu vya maabara kwa kasi ile ile iliyotumika kujenga shule za sekondari za kata.

Hata hivyo uchunguzi wa blog hii umebaini kuwa, pamoja na jitihada hizo za serikali bado shule nyingi za serikali zinakabiliwa na upungufu mkubwa wa walimu wenye uwezo wa kufundisha masomo ya sayansi

BARABARA KUU YA SINGIDA -MWANZA YAFUNGWA


Baadhi ya madereva wa masafa marefu na wananchi wa Munug'una, Singida vijijini wakiagalia daraja lililokatika na kusababisha msururu wa magari zaidi ya 200 kushindwa kupita mkoani Singida

Meneja wa TANROADS mkoa Singida Yustak Kangole(aliyeinama) akiwaelekeza wakandarasi wa kampuni ya CHICO kutathimini gharama ili walifanyie ukarabati na magari yaanze kupita

Mkuu wilaya Singida mwalimu Queen Mlozi (kushoto)akiteta jambo na RPC Singida Linus Sinzumwa katika eneo la daraja la kijiji cha Mnung'una, Singida vijijini kukatika na kusababisha magari kushindwa kupita

Mwalimu Queen Mlozi mkuu wilaya Singida akiwasiliana eneo lilikokatika daraja

Baada ya daraja Mnung'una kukatika, baadhi ya madereva wamebuni njia ya mzunguko, lakini pia ya hatari

 Dereva na msaidizi wake wakijipumzisha baada ya daraja la kijiji cha Munung'una barabara Singida-Nzega kukatika mkoani Singida, zaidi ya magari 200 ya abiria na mizigo yamekwama mkoani singida yakiwa safarini kuelekea maeneo mbalimbali ya tanzania na nchi jirani

HABARI NA PICHA ZOTE ZIMEPIGWA NA HALMA JAMAL


MVUA kubwa zinazoendelea kunyesha mkoani Singida,zimeendelea kuleta maadhara makubwa ikiwemo kuvunja daraja na barabara kuu ya Singida – Mwanza

Mvua hizo kubwa zilizoanza kunyesha mwanzoni mwa mwezi wa 12 mwaka jana,jana tar1 zilisababisha daraja la munung’una lililopo katika kijiji cha Msisi wilayani Singida,barabara kuu itokayo Singida kuelekea mikoa ya kanda ya ziwa na nchi jirani za Kongo,Burudi,Rwanda na Uganda, kubomoka na kusabaisha shimo kubwa.

Kubomoka kwa daraja hilo,kumesababisha foleni kubwa ya magari yanayokadiriwa kuwa ni zaidi ya mia tano.Pia mawasiliano kati ya mikoa mbalimbali ikiwemo ya kanda ya ziwa na nchi jirani,yamekatika.

Aidha mmoja wa madereva walioathirika na kubomoka kwa daraja hilo,George Medadi,aliyekuwa akitokea Mwanza akirudi jijini Dar-es-salaam,alisema daraja hilo limechangiwa kwa kiasi kikubwa na kujengwa chini ya kiwango.

Kutokana na hali hiyo wenyeji wa wa kijiji hicho wamesema kuwa kalvati zilizotumika kujengea daraja hilo,ni zile za zilizowekwa wakati wa uongozi wa Nalaila Kiula alipokuwa waziri wa ujenzi.

Wakifafanua zaidi wananchi hao walisema kuwa Kampuni ya CHICO iliyojenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami,waliyatumia makalivati hayo hayo na walichofanya ni kulundika udogo juu tu.

Naye dereva Iddi Mussa,alisema kuwa barabara nyingi zinazojengwa na kampuni za kichina,zimekuwa hazisimamiwi ipasavyo kitendo kinachochangia kuharibika haraka na kuisababishia serikali kuingia hasara kubwa.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Singida,mwalimu Queen Mlozi,alisema kwa kuanzia,wameimarisha ulinzi katika eneo hilo pamoja na kufungua kituo kidogo cha kutolea huduma ya afya na kuthibiti uwezekano wa kutokea kwa magonjwa ya mlipuko.

“Pia tumefungua barabara ya Singida-Ndago –Misigiri kwa ajili ya kutumiwa na mabasi ya abiria na ale yenye uzito chini ya tani kumi.Vile vile tunaangalia uwezekano wa kuangalia ni namna gani watu waliokwama,wanapata chakula”,alisema.

Meneja wa TANROADS mkoa wa Singida,mhandisi Yustaki Kangole,ambaye alifika na wahandisi wa kampuni ya CHICO,alisema kuwa wamekubaliana na CHICO kwamba wafukie shimo hilo kwa vifusi vya mawe makubwa ili barabara hiyo ianze kutumika mapema iwezekanavyo

“Kwa sasa tunafanya kazi hii ya muda na baada ya eneo hili kukauka,ndio ukarabati mkubwa utafanywa ili kuimarisha barabara hii muhimu kwa uchumi wa taifa”,alisema mhandisi Kangole.

Kwa mujibu wa mhandisi Kangole,barabara hiyo ilijengwa kwa kiwango cha lami na kampuni ya kichina ya CHICO na ilikabidhiwa kwa serikali mwaka 2008.

Wakati huo huo,mkuu wa wilaya ya Mkalama,Edward Ole Lenga,amesema kuwa raia moja wa nchini China,amefariki dunia baada ya gari lake kusombwa na maji ya mto kaka jirani na kijiji cha Gumanga

Alisema mchina huyo ambaye jina lake bado halijatambuliwa hadi sasa,alisombwa na maji ya mto juzi majira ya jioni wakati akikatisha mto wa kijiji cha Gumanga wilaya ya Mkalama.Ndani ya gari hilo mchina huo alikuwa na mtoto wake ambaye alinusurika kufa.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida,Linus Sinzumwa,alikiri kutokea kwa tukio hilo la mchina kusombwa na maji mto.


 

Tuesday, January 1, 2013

BEST WISHES FROM MANAGING DIRECTOR

 


On my behalf, Management and staff of STANDARD VOICE LTD & STANDARD RADIO FM 90.1 Singida, I hereby wish all listeners, Singida community and all Tanzanians a HAPPY & PROSPEROUS NEW YEAR 2013.

MPENDWA MSIKILIZAJI WA STANDARD RADIO FM

MIMI JAMES JAPHET DAUD, MKURUGENZI MTENDAJI WA MAKAMPUNI YA BUHANZO INTERPRISES LTD NA STANDARD VOICE LTD AMBAYE NI MMILIKI WA STANDARD RADIO FM SINGIDA

NINAPENDA KUCHUKUA FURSA HII KUKUPONGEZA SANA KWA KUUFIKIA MWAKA MPYA WA 2013, NINAWAOMBEA MWAKA HUU UWE WA AMANI, FURAHA, UPENDO NA UCHAPA KAZI UTAKAOLETA TIJA KWA MAENDELEOO YA MTU MMOJA MMOJA, KAYA, MKOA NA TAIFA KWA UJUMLA

MIMI PAMOJA NA WAFANYAKAZI WOTE WA MAKAMPUNI YA BUHANZO NA STANDARD, TUNAPENDA KWA NAMNA YA PEKEE KABISA KUTOA SHUKURANI ZA DHATI KWAKO WEWE MSIKILIZAJI WA STANDARD RADIO, WAKAZI WOTE WA MKOA WA SINGIDA, UONGOZI WA SERIKALI, MASHIRIKA YA UMMA NA TAASISI ZA KIJAMII PAMOJA NA VYAMA VYOTE VYA SIASA, KWA NAMNA MNAVYOIPOKEA NA KUISIKILIZA RADIO YETU.

NDUGU ZANGU UKARIMU WENU KWA STANDARD RADIO NI WA KIPEKEE KABISA, NINAPENDA KUKIRI KUWA UAMUZI WETU WA KUILETA RADIO HII MKOANI SINGIDA UMEENZIWA NA WANA SINGIDA VILIVYO, TUMEKUWA TUKIPOKEA MAONI MENGI AMBAYO YOTE YANADHIHIRISHA MAPENZI MEMA KWA RADIO HII

STANDARD RADIO NI RADIO YA JAMII, YENYE MALENGO YA KUCHOCHEA MAENDELEO YA JAMII KWA NJIA YA KUHABARISHA, KUELIMISHA NA KUBURUDISHA, MALENGO YETU NI KUISAIDIA JAMII KUIBUA NA KUTEKELEZA SHUGHULI ZA MAENELEO HUSUSANI KILIMO, BIASHARA, UJASIRIAMALI PAMOJA NA KUHIMIZA MASUALA YA ULINZI NA USALAMA KUPITIA KAULI MBIU YA ULINZI SHIRIKISHI NA UTII WA SHERIA BILA SHURUTI

JAMII INAPASWA KUPATA FURSA YA KUTOA YALIYO MOYONI ILI VYMBO VYA MAAMUZI VIYASIKIE NA KUYAFANYIA KAZI, JAMBO HILI NI GUMU KAMA HAKUNA CHOMBO MBADALA CHA KUFIKISHA SAUTI YA WANANCHI. HII NDIYO SABABU SISI TUMEKUJA SINGIDA ILI TUWE SAUTI YA WASIO SIKIKA, KAMA KAULI MBIU YETU INAVYO SEMA (THE VOICE OF VOICELESS)

STANDARD RADIO BADO IKO KATIKA MCHAKATO WA MWISHO KUELEKEA KUANZA MATANGAZO RASMI KWA MUJIBU WA TARATIBU ZA MAMMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA, KWA HIYO TUNAKUOMBA NDUGU MSIKILIZAJI UENDELEE KUWA NA SUBIRA KWANI WAKATII WOWOTE MATANGAZO YETU YATAANZA KUSIKIKA KWA NJIA YA VIPINDI MBALIMBALI.

SUBIRA YAVUTA KHERI, TUMEVUMILIA TANGU ENZI ZA UKOLONI NA BAADA YA UHURU MIAKA HAMSINI ILIYOPITA SINGIDA IKIWA HAINA RADIO, SASA TUSISHINDWE KUVUMILIA KIPINDI HIKI KIFUPI KIJACHO AMBACHO  STANDARD RADIO INAJIWEKA SAWA ILI KUKULETEA MATANGAZO KAMILI

NARUDIA TENA KUKUSHUKURU NA KUKUTAKIA MWAKA MPYA MWEMA

 
MUNGU AWABARIKI

SPECIAL LECTURE FROM STANDARD RADIO FOR NEW YEAR 2013

HAPPY NEW YEAR 2013

What Is a Healthy Radio Station?

By Boniface Mpagape.


By its nature, community radio is as diverse as the communities it serves.  At the same time, donors look for some measures of effectiveness.  These organizational benchmarks are useful guides to evaluate whether it is a Healthy Station.

Naturally, no radio template fits all communities; each country has a unique history, culture and legal framework.   These must be respected.  Radio serving a Maasai village of 1,800 in rural Tanzania will be very different than one serving a densely populated peri-urban township such as Soweto in South Africa.  Regardless of the differences, however, effective, healthy local radio stations have these benchmarks:

·      A clear mission that informs programming, advertising and outreach decisions.  Each staff member and volunteer understands this mission and uses it as a guide star.

·      A defined audience and ongoing engagement with that audience

·      A clear voice (or style of presentation) that is confidently and distinctively community radio.  The station does not copy or duplicate an existing service.

·      A community-wide reputation of being independent of outside influence and adhering to professional journalism standards of accuracy, fairness and balance in information programming.

·      Local content and music.

·      Strong and fair leadership combined with the ability to empower the staff by engaging them constructively.

·      On-going evaluation mechanisms to gauge effectiveness of programming, management and service to the community.

·      Open relations between stakeholders, including board, staff, donors, advertisers and listeners who encourage creative programming.

·      Financial independence.

·      An active board of directors that is engaged with the station and representative of the community.

·      A written code of ethics supported and used by staff and volunteers.

Now stations can use SMS text messaging as a new tool for community engagement by soliciting topics for programs and polling listeners to evaluate the programming.

One other quality I found that effective stations had in common was a culture of candor, of constructive self-criticism.  One station had adopted the Japanese idea of kaizen, continuous improvement.  Rather than hide problems, they bring them into the light so they can be fixed.  Criticism is not personal; rather it is in the interest of striving for excellence for the station as whole.

One last point: All too often donors, NGOs and governments focus on using media to bring information to people and under value the importance of dialogue or horizontal communication.  Radio is unique in giving voice to people to air and solve their problems, to hold public officials accountable, discuss taboo subjects and change harmful behavior.  This is the essence, of course, of Radio for Peace Building.

While stopping horrific violence with peacemaking remains a challenge in too many African countries, we can also take a new broader look at peace building.

We know that the ‘enemies’ in the world today are actually conditions - - poverty, infectious disease, political turmoil and corruption, environmental and energy challenges.

We know from our own experience and research that effective local radio programming can make significant progress to improve each one of these conditions.  Few other social investments can have broader reach or affect more lives than an effective local radio station.