Friday, April 26, 2013

SHEREHE ZA MUUNGANO NA MAPAMBANO DHIDI YA NJAA SINGIDA


Source: SR/Chami

Ed: BM

Date: 26 April 2013.

 

SINGIDA

 

Wananchi mkoani Singida wametakiwa kudumisha amani, upendo na ushirikiano bila kusahau kuhifadhi chakula ili kujikinga na baa la njaa

Akihutubia katika siku ya maadhimisho ya sherehe za muungano wa Tanganyika na Zanzibar,  ambayo kiwilaya imefanyika katika kata ya mandewa viwanja vya mandewa, Mkuu wa wilaya ya Singida Mwalimu Qeen Mlozi amesema ni vyema wananchi kutumia maadhimisho hayo katika  kutekeleza shughuli za kiuchumi.

Amesema ili kutekeleza shughuli za kiuchumi lazima iwepo amani na utulivu na kwamba ni jukumu la kila mwananchi kuzuia uuzaji wa mazao ya vyakula yakiwa shambani, tena kwa bei ya chini ama kuuza kwa ujazo usio sahihi badala yake watumie ujazo uliowekwa kisheria.

Ameongeza kusema kuwa muungano huu utumike kama kiashiria kizuri cha amani na utulivu katika shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii kwani kwa kufanya hivyo nchi itabadilika kimaendeleo.

Kauli mbiu ya mwaka huu ya maadhimisho ya sherehe za muungano ni amani,utulivu na maendeleo ni matokeo ya muungano wetu tuuenzi na kuulinda.

Thursday, April 25, 2013

VIJANA WAPEWA SOMO-MATUMIZI YA VIDHIBITI MIMBA


Source: SR/Monica

Ed: BM

Date: 25 April 2013.

 SINGIDA

Vijana wametakiwa kutojihusisha na matumizi ya vidhibiti mimba pasipo kujua madhara yake.

Hayo yamesemwa na Bi Judith Kattani mratibu wa Pro-life Tanzania jimbo la Singida na Kahama, alipokuwa akizungumza katika kipindi cha Hoja ya leo jana kinachotangazwa na Standard Radio.

Amesema kuwa vijana wengi wanaathirika na madawa hayo pasipo kujua kutokana na kukosa elimu ya kutosha.

 Bi Judith amesema kutokana na matumizi hayo ya vidhibiti mimba yanachangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa vijana kutokana na kuendekeza mapenzi na kujisahau katika utekelezaji wa majukumu yao.

 Mratibu huyo wa Pro-life Tanzania Bi Judith Kattani ametoa wito pia kwa wanafunzi kutojihusisha na vitendo vya mapenzi wakati wa masomo, jambo ambalo linachangia kwa kiasi kikubwa kushuka kwa kiwango cha elimu kutokana na matumizi hayo ya vidhibiti mimba yanayowafanya kujiamini kuwa hawawezi kupata mimba, jambo ambalo ni hatari kwao kwani huzuia mimba na kusahau kuwa kuna gonjwa la ukimwi.

 Aidha Bi Judith amewaasa wazazi kutoa ushirikiano kwa walimu ili kushirikiana kwa pamoja kuweza kuwalea watoto ili kukuza maadili ya vijana, kwani bila kufanya hivyo kiwango cha elimu kitazidi kushuka na maambukizi ya virisi vya ukimwi yatazidi kuongezeka.

CHANJO KWA WATOTO MKOANI SINGIDA

Na. Elisante John, Singida
 
WATOTO 997 Mkoani Singida wenye umri wa chini ya mwaka mmoja, wanatarajia kupata chanjo wakati wa wiki ya chanjo kitaifa, inayoendelea kufanyika nchini kote.

Hayo yamebainishwa na Mganga mkuu Mkoa wa Singida, Dk.Dorothy Kijugu na kubainisha kuwa jumla ya vituo 178 vitatumika kwa ajili ya kufanikisha zoezi hilo, lililoanza juzi Aprili 22 hadi 28, mwaka huu.



Naye mgeni rasmi katika uzinduzi huo uliofanyika leo kwenye kituo cha afya Sokoine Mjini Singida, Mwalimu Queen Mlozi amesifu jitihada zinazofanywa na wauguzi hadi kufikia mkoa kushika nafasi ya kwanza mwaka jana juu ya zoezi hilo na akawataka mwaka huu ushike nafasi ya kwanza.
Katika uzinduzi huo, Dk. Kijugu amesema kwa mujibu wa takwimu za shirika la afya Duniani (WHO) chanjo hizo kwa watoto chini ya mwaka mmoja zinazuia vifo takribani milioni mbili hadi tatu kila mwaka.