Wednesday, November 28, 2012

WAANDISHI WA HABARI SOMENI SERA KWANZA

Baadhi ya waandishi wa habari wa Kigoma Press Club (Picha na. Prosper Kwigize)


Waandishi wa habari nchini Tanzania wamepewa changamoto ya kuandika na kuchambua sera mbalimbali za serikali na mashirika ya kiraia ili kuisaidia jamii kutafsiri sera hizo kulingana na maisha yao ya kila siku

rai hiyo imetolewa na mwalimu Robert Renatus Mkufunzi wa mafunzo ya uchambuzi wa sera na ufuatiliaji wa bajeti yanayofanyika kwa waandishi wa habari mkoani Kigoma kwa ufadhili wa Umoja wa Vilabu vya waandishi wa habari Tanzania UTPC
Mwl. Robert Renatus, Mkufunzi na mwanachuo wa Chuo cha SAUT Mwanza


Mwalimu Renatus amebainisha kuwa, wandishi wasipojituma kuzijua na kuzichambua sera mbalimbali za taifa, itakuwa vigumu kwa watanzania kunufaika na habari nyingi zinazoandikwa bila kuwa na uchambuzi wa sera ya kile wanachoandika

kwa upande wao waandishi wa habari wanachama wa Klabu ya waandishi wa habari mkoani Kigoma wamekiri kuwepo kwa udhaifu mkubwa wa wanahabari kutoandika na kuchambua sera mbalimbali za maendeleo

Aidha wanahabari hao wamekiri pia kutozijua au kuzisoma sera mbalimbali za Tanzania

CHANGAMOTO KATIKA IDARA ZA AFYA-UWAJIBIKAJI DUNI


NA  Phesthow   sanga 
Shirika   lisilo  la kiserikali   {SIKIKA] ambalo  ofisi   yake  kuu  ipo  Dodoma   na  ambalo  linajihusisha  na mambo  ya   wizara  ya  Afya  nchini   hivi  majuzi   limemaliza   kazi  zake   za  Ufuatiliaji  wa  Uwajibikaji   jamii, katika  Uwajibikaji   wa  Watoa  huduma   na  wenye  Mamlaka  katika  kuhakikisha   haki  za  Binadamu   na   jamii   Zinapatikana .

 Timu  hiyo  ambayo  iliundwa  na wajumbe  waliochaguliwa  katika  makundi   mbali mbali  ya  jamii,wakiwepo  pia madiwani  wa  kamati  ya  Huduma  za  jamii  pamoja  na  Viongozi  wa  Dini  na  Madhehebu   yaliyopo   katika   wiliaya  ya  Iramba  walianza   kazi  tangu  Okt 25 na kumaliza nov 24  mwaka  huu.

Akiongea  na  Wanahabari,   Mkuu   wa  Ofisi  ya  Sikika  Dodoma   bw. Patrick N.Kinemo ,Amesema  kuwa  shirika   hilo katika   miaka yake   kumi  tangu  lianzishwe  limejikita  Na  mambo  ya  Wizara  ya  Afya  ikwemo  kufuatilia  mambo  ya  madawa, Raslimali Watu ,vifaa  Na  Mambo  yote  yanayohusu  wizara  ya  Afya  kwa  Ujumla  .

Akizitaja   kero  na  mapungufu  pamoja  na  mambo  mengine  yaliyoibuliwa   wakati  timu ya {PSAM} Ilipokuwa  ikitembelea  zahanati   Na  Vituo  vya  Afya   katika  wilaya  ya Iramba   Ni Pamoja  na  Akina mama  Wajawazito   kutozwa  gharama  za  Kadi   za  klinik  iwapo  mama  huyo  atakuwa  amepoteza  kadi  yake .

Hali hiyo ilkutwa  katika  Kituo  cha  Afya  cha  Mgongo  ambapo  Wananchi  walitoa  malalalmiko  yao  kuwa  wanalipizwa  tshs. Elfu Tano  kwa  mjamzito  kama  kapoteza  kadi  yake , pia  malalamiko kama  hayo  yalitolewa  na   wananchi  katika  Zahanati  ya  Shelui  kuwa   wajawazito   hulipizwa shilingi   Elfu  mbili  kama  amepoteza  kadi yake  huku  katika  kituo  cha  Afya  cha  Ndago  Akina mama hulipizwa  tshs Elfu moja  kwa  upotevu  wa  kadi.

 Mambo   Mengine  ni  Upungufu  mkubwa   wa  Watumishi , Uchakavu  wa  Majengo , magari  katika  Vituo  vya  Afya , Madawa , Vifaa Tiba,  Ulinzi , Usimamizi  wa Fedha ,matibabu ya  Wazee  mizani  za watoto katika  Zahanati nyingi , Semina  kwa  watoa  Huduma.

Aidha   Timu ya public  service  accountability  monitoring {PSAM}  Imegundua  madawa  ya thamani  ya tshs .1,342,400.yameharibika  na kutofaa  tena  katika  matumizi  ya  Binadamu  bado  Hayaja  teketezwa  na kuchomwa   kama  ilivyoagizwa  na  amri {order}  no.244  ya mwaka 1997  na  hakuna  hatua   zozote Zilizochukuilwa   na  Uongozi wa  Halmashauri  hiyo.

Kutokana  na  taarifa  ya  Timu  ya  PSAM,  Iligundua  pia  Akiba  kubwa  ya  Vyandarua  katika  stoo  ya hospitali   ya  wilaya  Neti  ambazo  hazijagawiwa ;4811 ambazo  zilitolewa  na MEDA , Tangu  Januari 2011; na  uongozi  wa Halmashauri  upo  na  hakuna  hatua  yoyote  ilyochukuliwa  kuhusiana  na vyandarua  hivyo .

Akijibu  na kutolea  Ufafanuzi   kuhusu  Taarifa  Iliyotolewa   na Timu  ya  psam   Kaimu  Mganga  Mkuu  wa  Wilaya  Dr.  Mbulu  alieleza  kuwa  katika  mambo yote  yaliyosemwa   yanatekelezwa  kulingana  na  bajeti ,aidha  alikiri  kuwa  mambo  Mengine Watayafuatilia ,kama  Utozwaji  wa  kadi  za  klinik  kwa  akina  Mama wajawazito

Tuesday, November 27, 2012

RIPOTI YA NCHI MASIKINII ZAIDI DUNIANI



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 

UNCTAD/PRESS/PR/2012/40*

Original: English

 

RIPOTI YA NCHI MASIKINI SANA DUNIANI MWAKA 2012

UKWELI WA MAMBO NA TARAKIMU

 

Geneva, 26 Novemba 2012

 

Ripoti ya  Nchi Maskini Sana Duniani ya Mwaka 20121, yenye kichwa kidogo cha habari

Kutumia Fedha Zinazotumwa na Raia Wanaoishi Nga’mbo na Weledi Wao Kujenga Uwezo wa Uzalishaji,

 

Mwelekeo wa uhamiaji

 

Ø  Idadi ya watu ambao wamehamia Ulaya kutoka Nchi Maskini Sana (LDCs) iliongezeka kutoka milioni 19 mwaka 2000 kufikia milioni 27 mwaka 2010. Hii ni sawa na 3.3% ya wakazi wote wa nchi hizo.

Ø  Nchi Maskini Sana Duniani  zinatoa 13% ya wahamiaji duniani kote---idadi ambayo inalingana na mgawo wa LDCs katika idadi ya wakazi wote duniani (12.1%).

Ø  Wahamiaji wanne kati ya watano kutoka LDCs wanaishi kwenye nchi zinazoendelea (Kusini) na mmoja tu kati wa watano ndiye anaishi kwenye nchi zilizoendelea (Kaskazini).

Utumaji fedha

 

Ø  Kiwango cha fedha zinazotumwa na raia waliohamia ng’ambo kwenda kwenye nchi zao kiliongezeka mara nane kati ya mwaka 1990 na 2011: Kutoka dola bilioni 3.5 kufikia dola bilioni 27. Tangu mwaka 2008 kiasi cha fedha kimeendelea kuongezeka pamoja na kuwepo na anguko la kiuchumi duniani.

Ø  Mwaka 2011 kiasi cha fedha zilizotumwa kwenda nchini Tanzania kutoka Uingereza zilikuwa dola milioni 4.5, kutoka Canada dola milioni 3.2 na kutoka Kenya dola milioni 2.5.

Ø  Mwaka 2011, fedha zilizotumwa kwenda LDCs zilikuwa kama mara mbili ya thamani ya uwekezaji wa moja kwa moja (FDI) katika nchi hizi (dola milioni 15), na kiwango hiki kilizidiwa tu na Misaada Rasmi  Kutoka Nje, yaani ODA (dola bilioni 42 mwaka 2010), kama chanzo cha fedha kutoka nje ya nchi.

Ø  Kiwango cha fedha zinazotumwa kutoka nje kama kingegawanywa kwa mwananchi mmoja mmoja kiliongezeka kutoka dola 10 kama kila mtu angepokea hadi dola 30 kati ya mwaka 2000 na 2010.

Ø  Fedha zinazotumwa na raia wanaoishi nje zina umuhimu wa pekee kwa LDCs ikilinganishwa na nchi zilizo katika makundi mengine. Katika LDCs, fedha zinazotumwa na raia kutoka nje zinachangia 4.4% kwenye pato la nchi na 15% ya thamani ya bidhaa zinazouzwa nje. Kiwango hiki ni kikubwa kwa mara tatu ikilinganishwa na nchi nyingine zinazoendelea (ambazo siyo LDCs).

Ø  Kuanzia mwaka 2008 hadi 2010, kiasi cha fedha kilichotumwa kutoka nga’mbo kinalingana na zaidi ya moja ya tano ya pato la taifa la nchi za Lesotho, Samoa, Haiti na Nepal.

Ø  Tangu mwaka 2009 hadi 2011, nchi za Nepal na Haiti zilipata fedha nyingi za nje kutoka kwa raia wao walio ng’ambo kuliko zile ambazo nchi hizi zilipata kutokana na mauzo ya bidhaa nje.

Ø  Kwa LDCs tisa, kiwango cha fedha zinazotumwa na raia wanaoishi nje kilizidi kile cha uwekezaji wa moja kwa moja kutoka nje (FDI) na misaada rasmi kutoka nje  (ODA) kati ya mwaka 2008 na 2010. Hizi ni nchi za Bangladesh, Haiti, Lesotho, Nepal, Samoa, Senegal, Sudan, Togo na Yemen. Kwenye nchi nyingine nane za kundi la LDCs, katika kipindi hicho hicho, fedha zinazotumwa na raia kutoka ng’ambo zilizidi FDI: Benin, Burundi, Comoros, Ethiopia, Gambia, Guinea-Bissau, Kiribati na Uganda.

Ø  Theluthi mbili ya fedha zinazotumwa na raia kutoka ng’ambo kwenda kwenye LDCs zinatoka kwenye nchi zinazoendelea.

Ø  Duniani kote, gharama ya kutuma fedha zinafikia 9% ya kiwango cha fedha kilichotumwa; kwa LDCs gharama ni kubwa zaidi kwa theluthi moja (12%).

Ø  Kama nchi zilizo kusini kwa Jangwa la Sahara zingelipia gharama za uhamishaji fedha kwa wastani wa gharama inayolipwa duniani kote, mapato yao yangekuwa yaliongezeka kwa dola bilioni 6  mwaka 2010.

Ø  Asilimia 66 ya fedha zilizohamishwa kwenda kwenye LDCs kati ya mwaka 2009 na 2011 ni za nchi tatu tu: Bangladesh, Nepal na Sudan.

Ø  Matumizi ya simu za mkono kwenye LDCs ni makubwa zaidi (368 kwa kila wakazi 1,000)  kuliko idadi ya akaunti za benki (171 kwa wakazi 1,000). Simu za mkono zinaweza vile vile kutumika katika kuhamisha na kupokea fedha kutoka ng’ambo.

 

Kuhama kwa utaalam                                    

 

Ø  Mtu mmoja kati ya kila watu watatu wenye ujuzi mkubwa (mwenye elimu ya chuo kikuu) kutoka LDCs anaishi ng’ambo. Kwenye nchi zilizoendelea kiwango ni mtu mmoja katika kila watu 25.

Ø  LDCs sita zina raia wao wataalaum wengi zaidi wanaoishi nje ya nchi kuliko wale waliobakia nchini mwao: Haiti, Samoa, Gambia, Tuvalu na Sierra Leone.

Ø  Theluthi mbili ya wahamiaji wenye ujuzi mkubwa kutoka LDCs wanaishi kwenye nchi zilizoendelea; theluthi moja wanaishi katika nchi zinazoendelea.

Ø  Kiwango cha kuhama kwa watu wenye ujuzi kwenda ng’ambo ni kikubwa (20% ) kwa LDCs nyingi (30 kati ya 48).

Ø  Wahamiaji kutoka LDCs wenye elimu ya chuo kikuu ambao wanaishi na kufanya kazi ng’ambo inafikia milioni 2.

Ø  Idadi ya Watanzania waliohamia Uingereza kwa kumbukumbu za mwaka 2000 ni 10,535.

Ø  Aina ya wahamiaji inafuata ukubwa wa kipato wa nchi mwenyeji. Katika nchi zilizoendelea, 35% ya wahamiaji ni wale wenye elimu ya chuo kikuu; kwenye LDCs 4% tu ya wahamiaji wana kiwango hicho cha elimu. Viwango hivi ni kwa wahamiaji kutoka nchi zote, japo viwango ni hivi hivi kwa wahamiaji kutoka nchi za kundi la LDCs.

Ø  Theluthi moja ya wahamiaji kutoka LDCs ambao wana elimu ya chuo kikuu wanaishi Marekani.

 

 

Uwezo wa kiuchumi (Uchumi mpana)

 

Ø  Kiwango cha ukuaji wa uchumi kwa mwaka kwa LDCs tangu kipindi cha msukosuko wa kiuchumi duniani (2009-2011) ni 4.7%, ambacho ni chini ya kiwango cha kipindi cha miaka ya ukuaji mkubwa wa kiuchumi (2003-2008), yaani 7.9%. Hii ina maana kwamba kiwango cha ukuaji wa kipato kwa mwaka kwa kila mkazi kilishuka kutoka 5.4% miaka ya ukuaji mzuri wa uchumi hadi kufikia 2.4%.

Ø  Wastani wa ukuaji halisi wa pato la nchi katika LDCs mwaka 2011, yaani 4.2%, ulikuwa chini ya 4.9% ya mwaka 2009 wakati wa anguko la uchumi duniani.

Ø  Kile kinachojulikana kama Gross fixed capital formation kwenye LDCs kilipanda kidogo kutoka 20.7% ya pato la jumla la taifa mwaka katika miaka ya 2005-2007 kufikia 21.6% miaka ya 2008-2010. Hata hivyo, bado kilibaki chini ya viwango vya nchi nyingine zinazoendelea, ambazo zilifikia kiwango cha 30.1%.

Ø  LDCs zinaendelea kutegemea sana raslimali kutoka nje. Pengo la pato linalotokana na uagizaji bidhaa na uuzaji bidhaa nje lilikuwa kubwa kwa 20% ya pato la jumla la taifa katika nchi tano za kundi la LDCs mwaka 2011, wakati LDCs nyingine 13 pengo lilikuwa asilimia 10 ya pato la jumla la taifa.

Ø  Kiwango cha utegemezi wa rasilimali kutoka nje katika kulipia uwekezaji wa ndani ya nchi kati ya mwaka 2008 na 2010 kilikuwa 15% ya pato la jumla la taifa kwa LDCs ambazo hazisafirishi mafuta nje.

Ø  Asilimia 62 ya mauzo ya bidhaa nje kutoka LDCs 48 yalikuwa ni kutoka nchi tano tu: Angola, Bangladesh, Equatorial Guinea, Yemen na Sudan. Ukiacha Bangladesh, nchi zote hizi zinauza mafuta nje.

Ø  Mapato ya LDC kwa mauzo ya bidhaa nje yanategemea zaidi mauzo ya bidhaa moja (mafuta), ambayo yanaingiza 46% ya jumla ya mapato yote yanayotokana na mauzo ya bidhaa nje.

Ø  Zaidi ya nusu ya mauzo ya nje kutoka LDCs (54%) yalikuwa yanakwenda kwenye nchi zinazoendelea mwaka 2011, mwelekeo unaothibitisha umuhimu wa biashara ya kusini-kusini. China ndiyo iliyonunua bidhaa nyingi zaidi kutoka LDCs (26.4%) ikiwazidi Jumuia ya Ulaya (20.4%) na Marekani (19%).

 

ZIKO WAPI NCHI MASKINI SANA DUNIANI?

Umoja wa Mataifa unaziweka nchi 48 kwenye kundi la Nchi Maskini Sana Duniani (LDCs). Mgawanyo wao ni kama ifuatavyo.

 

Africa (33):        Angola, Benin, Burkina Faso, Burundi, Central African Republic, Chad, Comoros, Jamhuri ya KIdemnokrasia ya Kongo(DRC), Djibouti, Equatorial Guinea, Eritrea, Ethiopia, Gambia, Guinea, Guinea-Bissau, Lesotho, Liberia, Madagascar, Malawi, Mali, Mauritania, Msumbiji, Niger, Rwanda, Sao Tome na Principe, Senegal, Sierra Leone, Somalia, Sudan, Togo, Uganda, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Zambia;

Asia (9):             Afghanistan, Bangladesh, Bhutan, Cambodia, Lao, Myanmar, Nepal, Timor-Leste na Yemen;

Caribbean (1):    Haiti;

Pacific (5):          Kiribati, Samoa, Solomon Islands, Tuvalu na Vanuatu.

Mchoro 1 – Nchi 48 za kundi la LDCs

 

Imetolewa na UNCTAD

 

Kutengeneza list ya LDCs

 

List ya LDCs inapitiwa upya kila baada ya miaka mitatu na Baraza la Uchumi na Jamii (ECOSOC) la Umoja wa Mataifa, kufuatana na mapendekezo ya kamati ya Sera ya Maendeleo (CDP).

Katika mapitio ya hivi karibuni, Machi 2012, CDP ilitumia vigezo vifuatavyo:

1.      Kigezo cha pato la kila mtu, kwa kufuata Pato la Jumla la Nchi (GNI) kwa kila kichwa (wastani wa miaka mitatu)

2.      Kigezo cha raslimali watu ambacho kinatumia viashiria kama lishe, afya, kuandikishwa shuleni na kujua kusoma na kuandika

3.      Kigezo cha mazingira hatarishi ya kiuchumi. Ambacho kinatumia viashiria kama mishtuko ya kiasili, mishtuko ya kibiashara, udogo na umbali.

Nchi tatu tu zimefanikiwa kupanda daraja kutoka list ya nchi za kundi la LDCs: Botswana Desemba 1994, Cape Verde   Desemba 2007 na Maldivs Januari 2011. Samoa inategemewa kupanda daraja tarehe 1 Januari 2014.

 

ECOSOC ilipitisha pendekezo la CDP kuipandisha daraja Equatiorial Guiones mwezi Julai mwaka 2009 na mwezi Julai 2012 ikakubali pendekezo la CDP kuipandisha Vanuatu. Hata hivyo ruhusa ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa bado itahitajika ili kuzipandisha daraja nchi hizi mbili.

 

 



* Contacts: UNCTAD Communications and Information Unit, +41 22 917 5828, +41 79 502 43 11, unctadpress@unctad.org, http://unctad.org/en/pages/Media.aspx

Saturday, November 24, 2012

ALBINO WAOMBA ULINZI ZAIDI TANZANIA


Na  Phesthow  Sanga

Walemavu  wa  ngozi [ALBINO}  Mkoani  Singida  Wameshauriwa  Kujitambua  na Kukubali  hali  Waliyonayo,  kuwa  ni  sawa  na  Watu  Wengine  Wenye  Ngozi  Nyeusi  kote  duniani.

Wito  huo umetolewa na  Ofisa  Ustawi  wa Jamii  Emanuely  Mramba  kwa  niaba  ya  Mkuu  wa  Wilaya  ya  Iramba  Yahya  Nawanda,  katika  Mdahalo  wa chama  cha  maalbino Mkoa wa Singida ,watumishi wa Serikali, Viongozi  wa Dini  na Wadau Wengine  uliofanyika  katika  ukumbi wa Halmashauri ya  wilaya  ya  Iramba.
 

Akisoma Risala kwa  Mgeni  rasmi  katibu  wa Albino  Mkoa wa Singida  Mwanahamisi  Msembo, alisema kuwa  chama  cha Albino  Mkoa wa Singida kilianzishwa  Septemba mwaka 1991 na aliyekuwa  katibu mkuu wa chama hicho marehemu Hamisi maimu kukiwa  na albino  15 tu.
 

Mwanahamisi  alijuza  kuwa  mpaka  sasa  Mkoa  wa  Singida  Unawana chama 338 waliosajiliwa na waliosambaa katika wilaya  zote nne za mkoa wa Singida.

Aidha  Mdahalo huo, ulikuwa Unahoji  kuhusu Ushirikishwaji  wa  watu  wenye Ualbino  katika  shughuli  za  kimaendeleo  ngazi  za  wilaya  mkoani singida,ki-afya ,elimu ,pamoja  na  Ulinzi na Usalama katika  maeneo yote walipo albino kutokanan na vitisho na changamoto  zote zinazowakabili.

Akijibu hoja za Afya kaimu mganga mkuu wa hospitali ya wilaya  Dr.JabirJuma alisema kuwa hospitali yake Imeweka mikakati  dhabiti  ya kupata daktari pamoja  na kilniki ya watu wa Ulemavu wa ngonzi katika  wilaya  ya  Iramba kwa muda  mfupi  ujao .

Hata hivyo kwa  upande wa Elimu ofisa elimu maalum Iramba Bw. Mathew Njoghomi  aliwaeleza  wanamdahalo  kuwa  Idara  yake  inatoa  Elimu  kwa walemavu  wa ngozi {Albino} katika  shule ya Kizega sawa na watoto  wengine  pia wanapewa  Ulinzi wakutosha  wakati wote kutoka kwa jeshi la Polisi pamoja na Jamii

UTPC YATOA VIFAA KWA PRESS CLUBS TANZANIA


Muungano wa vilabu vya waandishi wa habari Tanzania umetoa vifaa vya kazi (vitendea kazi) vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 35 kwa kila klabu ya wanahabari kwa lengo la kuboresha utendaji kazi, weledi na kujenga uchumi wa vilabu hivyo

Akikabidhi vifaa hivyo kwa klabu ya waandishi wa habari mkoa wa Kigoma, vifaa ambavyo ni pamoja na kamera, computer, runinga na zana za kisasa za mikutano na semina (projector), Rais wa UTPC Bw. Kenny Simbaya amehimiza utunzaji wa zana hizo pamoja na nidhamu ya matumizi
Bw. Kenny Simbaya Rais wa UTPC

Bw. Simbaya ameeleza kuwa zana hizo ni matokeo ya utekelezaji wa mradi wa kuimarisha Press Club nchini, mpango ambao umefadhiliwa na mradi wa maendeleo wa Ubalozi wa Sweeden Tanzania
Baadhi ya waandishi wa habari wa Klabu ya Waandishi wa habari mkoani Kigoma wakiwa katika mkutano mkuu maalumu wa marekebisho ya Katiba yao, mkutano huo ulihudhuriwa na pia na Rais wa UTPC Bw. Kenny Simbaya ambaye pia alikabidhi zana za kazi

Tanzania ina jumla ya Vilabu vya waandishi wa habari 23 hadi sasa na upo uwezekano wa kuongezeka kufuatia serikali kuongeza idadi ya mikoa nchini

JACKTON MANYERERE NA HUKUMU YA KIFO


Jackton Manyerere Mwanahabari mwandamizi na Mhariri wa gazeti la JAMHURI

Wiki hii Blog hii iliweka taarifa ya msimamo na maelezo ya katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban ki-moon kuhusu hukumu ya kifo, habari hiyo imesomwa na watu wengi ndan na nje ya afrika na wengi wamekuwa na hoja nyingi kuhusu hukumu ya kifo. haya hapa chini ni maoni ya Ndg MANYERERE
 

Hawa jamaa wa UN wasitake kutuchezea akili. Adhabu ya kifo ni mbaya, sawa; lakini inastahili. Nimepata kumhoji Jaji Samatta juu ya adhabu hiyo, yeye anaiunga mkono.

 

Hoja yake ni kwamba kuna kesi ukiisikiliza, ukajua namna mhusika alivyoshiriki kumuua binadamu mwenzake, kama kweli ni Jaji mtenda haki, atamhukumu adhabu ya kifo.

 

Juzi hapa wanajeshi wamehukumiwa kifo kwa kumuua Swetu. Hawa watu ukiwakuta mitaani wanavyoadhibu binadamu wengine hadi kuwaua, hakika huwezi kuwaonea huruma nao wanapohukumiwa.

Fikiria, majambazi wanaingia nyumbani kwako na kuiua familia yako, kisha wanaambulia kuchukua sh laki moja, au kuku, au mbuzi. Katika mazingira kama hayo, wahusika wakipatikana hakuna adhabu sahihi kwao zaidi ya kunyongwa, tena si kunyongwa tu, bali kunyongwa hadi kufa.

Kama kweli UN wanaona adhabu hii haifai, basi waanze na wafadhili wao wakuu, "mabwana" wa demokrasia-Marekani ili nao waache kufanya hivyo. Saddam Husseina alinyongwa, Gaddafi kauawa na wakala wao Wamarekani na Wafaransa; iweje kuwaua hawa iwe halali, lakini sisi kuwanyonga wanaowanyonga ndugu zetu iwe si haki?

Afrika Kusini walijipendekeza kufuta adhabu hiyo kwa busara zas Jaji Mwalusanya wa Tanzania. Sasa wanajuta! Wanataka adhabu ya kifo irejeshwe maana ushenzi umepindukia nchini humo.


Tuache kuimba wimbo wa UN pamoja na asasi za kiraia ambazo kazi yake ni kusaka fedha. Adhabu ya kifo inawafaa sana wale wanaoistahili. Haki ya kuishi isiwe kwa muuaji tu, bali tutazame na yule aliyeuawa anatendewa haki vipi!


Manyerere

Nawasilisha

 

Wednesday, November 21, 2012

UN STATEMENT BY BAN KI-MOON ON DEATH PENALT


  U N I T E D   N A T I O N S                                              N A T I O N S   U N I E S

 

 

 

 

Statement by the UN Secretary-General, Ban Ki-moon on the adoption by the General Assembly’s Third Committee of the resolution “Moratorium on the use of the death penalty”



NEW YORK, 21 November: The UN Secretary-General, Ban Ki-moon welcomes Monday’s (                            19November 2012) record vote in favour of the call for a moratorium on the use of the death penalty by the Third Committee of the General Assembly, which adopted the resolution by 110 votes in favour (with 39 against and 36 abstentions). The new resolution, inter alia, calls on all States to establish a moratorium on executions with a view to abolishing the death penalty. It reflects a trend against capital punishment which has grown stronger across regions, legal traditions and customs since the landmark resolution of the General Assembly in 2007. The Secretary-General saluted this development at a high-level event on the death penalty in New York this July. He said then that the taking of life is too absolute, too irreversible, for one human being to inflict on another, even when backed by legal process.

Some 150 States have either abolished or do not practice the death penalty. Yesterday’s vote offers the opportunity to again encourage Member States who still practice the death penalty or retain it in law to follow suit. The Secretary-General therefore calls on Member States to join the worldwide trend and support next month’s General Assembly resolution on a moratorium on the use of the death penalty.



New York,
21 November 2012

SINGIDA PRESS CLUB YAPATA VIFAA VIPYA


 Na Evarista Lucas

Singida 

Nov 21,2012  

Klabu ya Waandishi wa Habari Singida(SINGPRESS) mapema wiki hii imepokea vifaa vya  ofisi vyenye thamani ya shilingi milioni thelathini na tano kwa ajili ya matumizi ya ofisi na ikiwa utekelezaji wa mpango mkakati wa Muungano wa Klabu  za Waandishi wa Habari Tanzania(UTPC).

Akikabidhi vifaa hivyo  mapema wiki hii kwa uongozi wa SINGPRESS; Afisa Programu, mahusiano ya Klabu na ufuatiliaji; Bwana Victor Maleko alisema; “Vifaa hivi tulivyoleta  ni kwaajili ya kuziwezesha Klabu za Waandishi wa habari nchini kuweza kujiendesha zenyewe kwa kutumia vifaa hivi ambavyo vitakuwa kama chanzo cha mapato ya Klabu. Pia ni utekelezaji wa mpango mkakati waUTPC na mkataba uliotiwa  saini na Klabu wanachama ikiwemo mafunzo yanayoendelea kutolewa na UTPC.”

Wakielezea kufarijika kwao na kupatiwa vifaa hivyo; baadhi ya viongozi wa SINGPRESS wamesema kuwa hiyo ni hatua moja kubwa sana kwa Klabu na wanachama wa SINGPRESS kwa ujumla. “ Tutapata na kuongeza kipato  cha Klabu kupitia mmradi wa huduma ya steshenari na ukodishaji wa vifaa mbali mbali vya Klabu kama kamera na vinasa sauti hata projekta.” Alisema kaimu katibu Mtendaji wa SINGPRESS Bwana Elisante John.

 Baadhi ya Vifaa vilivyopokelewa katika ofisi ya SINGPRESS ni pamoja na kamera ya picha za mnato, vidadavuzi, projekta, kinasa sauti, mashine ya  kutolea kopi, video(TV Flat Screen) deki ya DvD ,na  mashine ya kuchomea (laminator) vyenye thamani ya shilingi milioni thelathini na tano tu.

Kwa upande mwingine licha ya kupata vifaa hivyo ambavyo vitawasaidia katika utendaji kazi wao wa kila siku; wanachama wa SINGPRESS wamekuwa wakinufaika na mafunzo mbali mbali yanayoendelea kutolewa na MUungano wa Klabu za Waandishi wa Habri Tanzania ikiwa ni utekelezaji wa mpango mkakati na hati ya makubaliano baina ya UTPC na SINGPRESS uliotiwa saini mnamo mwaka jana.

 

RUSHWA INAZITAFUNA HALMASHAURI NCHINI TANZANIA


Baada ya kubaini na hatimae kukiri kuwa idara za serikali za mitaa zinanuka kwa rushwa nchini Tanzania Taasisi ya kuzuia na kupambana na rusha nchini TAKUKURU imeanza kutoa mafunzo kwa kamati za maadilii za halmashauri za wilaya, manispaa, miji na majiji nchini

Mkoani Kigoma mafunzo hayo yameanza jana yakihusisha kamati za maadili kutoka miko aya Kigoma, Kagera na Shinyanga ambapo zaidi ya washiriki 30 wamehudhuria mafunzo maalumu ya mkakati wa pili wa kupambana na Rushwa NASCAP II

Jumla ya halmashauri kumi na moja (11) zimetuma wawakilishi kushiriki mafunzo hayo

Cha kujiuliza ni je, kamati hizi za maadili zina nguvu gani ya kisheria ya kudhibiti vitendo vya rushwa miongoni mwa watumishi wa serikali za mitaa ambao wanatajwa kujilimbikizia mali kuliko hata kiwango vha mishahara yao na umri katika utumishi?

Je ni nani mteuzi wa kamati hizi ambazo miongoni mwa wajumbe wake nao ni watuhumiwa wa vitendo vya uvunjifu wa maadili, uzembe kazini na Rushwa?

Je! Kanuni ya uhakiki wa mali za watumishi ambayo imekuwa ikiwaandama wabunge na mawaziri, huku chini inatumika kudhibiti utajiri wa ghafla mara tu mtu anapopata ajira au uwakilishi wa wananchi katika halmashauri za wilaya, miji, manspaa na Jiji?

Hebu tuchangie hoja hii,

“kwa kuwapa mafunzo wajumbe wakamati za maadili za halmashauri, TAKUKURU itafanikiwa kudhibiti Ruswa katika ofisi za utoaji wa huduma kwa wananchi hususani idara ya Mipango, Utumishi, Ugavi, fedha na Afya? “

Tuma maoni yako kupitia srfm2011@gmail.com au tuma maoni yako kwenye kisanduku cha maoni chini ya habari hii, pia unaweza kupiga simu namba 0786200518 au 0763837396

UNAO UHURU WA KUSEMA CHOCHOTE NASI TUTAPEPERUSHA MAONI YAKO KWA UMAKINI

STANDARD RADIO FM

SAUTI YA WASIO SIKIKA